Naibu Waziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dkt.
Hamis Kigwangalla amesema kuwa atawaweka hadharani wanaume wote
wanaojihusisha na mapenzi ya jinsi moja (mashoga) ambao hufanya biashara
hiyo kupitia mitandao ya kijamii.
Naibu Waziri aliyasema hao jana usiku kupitia ukurasa wake wa Twitter
ambapo alieleza kuwa yupo katika ziara jimboni kwake na mara
atakaporejea jijini Dar es Salaam kabla ya kuhamia Dodoma rasmi ataiweka
orodha hiyo hadharani.
Aidha, amesema kuwa wale wote wanaodhani kuwa vita dhidi ya wanaume
wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja ni mzaha, wataona hali
itakavyokuwa kwani vita hiyo ni kubwa sana na wataishinda.
Kigwangalla ambaye pia ni mtaalamu wa afya alisema kuwa suala la mtu
kuwa shoga si suala la kibaolojia (asili) bali ni watu tu kujiendekeza
na hivyo watakahikikisha wanalikomesha.
Sheria ya ndoa ya Tanzania inapinga watu wa jinsia moja kujihusisha na
mahusiano ya kimapenzi, lakini pia ni kitu kilichozuiliwa katika vitabu
vitakatifu vya dini.
Dr. Kigwangalla,
Uchunguzi dhidi ya watuhumiwa wa ushoga unaendelea. Watakamatwa kimya
kimya! Serikali ina mkono mrefu. Wakipatikana watatusaidia wenza wao!
Dr. Kigwangalla,
Kuna watu wanadhani vita dhidi ya ushoga ni ya mzaha, ni vita kubwa na
tutaishinda. Mtandao ni mrefu na nitaendesha operation kamata kamata!
Dr. Kigwangalla, H.
Namalizia ziara jimboni. Nikirudi Dar, kabla ya kuhamia rasmi Dodoma,
nitaweka wazi orodha ya watuhumiwa wa ushoga wanaojiuza mitandaoni!
Dr. Kigwangalla, H.
Kuna nchi marafiki zetu zinafanya jitihada za kupenyeza ushoga Tanzania
na kudai ni haki ya binadamu kuchagua ampendaye, sisi tunasema NO!
Dr. Kigwangalla, H.
Ushoga hauna addiction wala siyo wa kuzaliwa nao, wanaofanya hivyo
wanajiendekeza tu! Ushoga siyo biological. Mashoga wote waache mara moja
Jumatano, 15 Februari 2017
Home »
» Naibu Waziri wa Afya kuweka hadharani majina ya mashoga Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Afya kuweka hadharani majina ya mashoga Dar es Salaam
Related Posts:
Baada ya Video Inayodhaniwa ni ya Mwanae Kusambaa Ikimuonyesha Akifanya Mapenzi na Jibaba,Kajala Afunguka Haya Mapya..!!!1 Muigizaji wa Filamu Tanzania Kajala Masanja amewafungukia wanaomsema kwamba ameshindwa kumlea binti yake ' Paula' na kusema anatamani awaoneshe watu hao malezi anayompatia binti yake huyo. Akipiga story na eNewz,… Read More
Lissu aachiwa kwa dhamana ya bondi ya Sh10mDar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo (Ijumaa) imemuachia, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) kwa dhamana ya bondi ya Sh10 milioni.Lissu amedhaminiwa na maelezo ya awali yatasomwa Aprili3, m… Read More
Alikiba Kuweka Muziki Wake Wasafi.com ni Sawa na Safari ya Mwezini..!! Kwa takribani miaka mitatu sasa mafahari wawili wa muziki wa kizazi kipya yaani Bongo Flava Alikiba na Diamond Platinumz wamekuwa katika bifu zito sana, licha ya wao kujaribu kila siku kuukwepa ukweli huo. Hakuna kati yao… Read More
Mwanamitindo afariki dunia kwa kugongwa na treni Mrembo wa miaka 19 aliyefahamika kwa jina la Fredzania Thompson amegongwa na treni wakati akipiga picha.Fredzania alikuwa ni mwanafunzi wa chuo cha Blinn na alikuwa na ndoto za kuwa mwanamitindo mkubwa duniani. Mzazi wa mrem… Read More
Kama Huwezi Kuachana Naye Usijaribu Kuchungulia Mawasiliano Yake....!!! Kuna siku nilijifanya Mjuaji nikadukua mawasiliano ya mchepuko wangu niliyokutana nayo huko sasa ni hatari tupu, sms ya kwanza kuingia jamaa anampongeza kwa shughuli yao ya jana kuja huku whatsaap shughuli nzito nikajikut… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni