Pamoja na wenyewe kudai hawajui kilichotokea, mastaa wawili wenye
sura za mauzo kunako sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Wema
Isaac Sepetu, kwa sasa wanadaiwa kufikia pabaya kufuatia bifu zito
linalofukuta kati yao.
Habari za mjini zinadai kwamba, Wema amekuwa akishtushwa na kuchukizwa
na kitendo cha Lulu kuwa upande wa aliyewahi kuwa mwandani wake, Nasibu
Abdul ‘Diamond Platnumz’ kiasi cha kwenda nyumbani kwake, Madale-Tegeta
jijini Dar, usiku wa manane na kujiachia na jamaa huyo anavyotaka.
“Kama mtakumbuka, kabla ya kifo cha Kanumba (Steven), Wema na Lulu
walikuwa ni mashosti kama ilivyokuwa kwa Wema na Snura (Mushi) au Wema
na Kajala (Masanja) au Wema na Aunt (Ezekiel).
“Lakini baada ya jamaa (Kanumba) kuondoka na kisa kizima cha Lulu ndipo
Wema akavunja urafiki na Lulu kwa sababu Kanumba aliwahi kuwa ‘mtu’ wa
Wema kama ilivyo kwa Diamond.
“Ulipita ukimya wa muda mrefu bila Wema na Lulu kuwa mashosti zaidi ya salamu.
“Lakini mambo yalianza tena kuwa mabaya baada ya Lulu kumponda Wema
alipokuwa akigombea Ubunge wa Viti Maalum kupitia CCM (Chama Cha
Mapinduzi).
“Sasa hivi ishu ni kitendo cha Lulu kujiachia na Diamond kwenye birthday
ya Rome Jones (binamu na DJ wa Diamond) kisha ile pati ya birthday
Diamond kuifanyia nyumbani kwake huku (Lulu) akitupia picha za mafumbo
yaliyoelekezwa kwa Wema.
“Hicho ndicho kinachoendelea na unaambiwa hali ni tete mno,” kilisema chanzo hicho ambacho ni mtu wa karibu wa mastaa hao.
Baada ya kupata ‘ubuyu’ kamili, Amani lilimtafuta Wema na kummwagia data
ambapo alionesha kushtushwa na kudai kwamba hata yeye anashangaa ni
nini kimetokea.
Kwa upande wake Lulu hakupatikana hewani lakini kwa mujibu wa mahojiano
aliyofanya hivi karibuni juu ya uhusiano wake na Wema, mwanadada huyo
alikiri kuwa rafiki wa Wema kitambo hicho lakini akasema hajui ni nini
kilichotokea zaidi ya kwamba huwa wanasalimiana tu wanapokutana.
Kabla ya mambo kwenda mrama, Lulu na Wema walikuwa mashosti wakubwa
ambapo gazeti hili liliwahi kuwashuhudia wakiwa lokeshi na kulala pamoja
chumba kimoja kama mtu na dada au mtu na mdogo wake.
Chanzo: GPL
Ijumaa, 16 Oktoba 2015
Home »
» LULU, WEMA WAFIKA PABAYA..KISA UHUSIANO NA DAIMOND ..
LULU, WEMA WAFIKA PABAYA..KISA UHUSIANO NA DAIMOND ..
Related Posts:
Laurence Masha Ajitoa Kugombea Urais TLS, Amuunga Mkono Tundu Lissu Mgombea Urais wa Chama cha Wanasheria nchini (TLS) Ndg. Laurence Masha amejitoa kwenye kinyang'anyiro hicho kwa hoja kuwa anaamini uwezo wa Lissu katika kuiongoza TLS.Amewaomba mawakili wote waliopanga kumpigia kura wampigie… Read More
Fahamu Maajabu ya Nanasi Ambayo Yatakuacha Kinywa Wazi..!!! BAADHI ya watu wamekuwa wakidai tunda la nanasi kuwa siyo salama kwa akina mama wajawazito, ingawa suala hili bado halijathibitishwa kitaalamu, kwani wapo wanaokula na haijawahi kuripotiwa madhara. Linatumika kama tunda… Read More
Lissu aachiwa kwa dhamana ya bondi ya Sh10mDar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo (Ijumaa) imemuachia, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) kwa dhamana ya bondi ya Sh10 milioni.Lissu amedhaminiwa na maelezo ya awali yatasomwa Aprili3, m… Read More
Ndoto za Mbwana Samatta Kucheza na Mau United Zawekwa Pending Ndoto za mshambuliaji wa timu ya KRC Genk ya Ubelgiji Mtanzania Mbwana Samatta za kukanyaga katika dimba la Old Trafford la Manchester United zimesubirishwa baada ya matokeo ya droo ya robo fainali kombe la Europa kwenda k… Read More
Baada ya Video Inayodhaniwa ni ya Mwanae Kusambaa Ikimuonyesha Akifanya Mapenzi na Jibaba,Kajala Afunguka Haya Mapya..!!!1 Muigizaji wa Filamu Tanzania Kajala Masanja amewafungukia wanaomsema kwamba ameshindwa kumlea binti yake ' Paula' na kusema anatamani awaoneshe watu hao malezi anayompatia binti yake huyo. Akipiga story na eNewz,… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni