Siku moja baada ya kutangaza kujitoa CCM, kada mkongwe wa chama hicho,
Balozi Juma Mwapachu amesema uamuzi alioufanya ni sahihi ambao hata Baba
wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere angekuwa hai angeufanya kwa sasa.
Balozi Mwapachu alieleza hayo jana katika mahojiano maalumu na kuongeza
kuwa chama chake cha zamani kimepoteza mwelekeo kwa kuwa kinara wa
kuvunja katiba na taratibu kitendo ambacho Nyerere alikichukia katika
maisha yake.
Alisema anafahamu fika kuna watu watakosoa uamuzi wake huo lakini
hatababaishwa na maneno yao na atasimamia msimamo wake huo huku akieleza
kuwa anajisikia amani kujitoa katika siku ya kumbukumbu ya miaka 16 ya
kifo cha Nyerere.
Mwapachu alitangaza kujitoa CCM juzi akisema kilivunja taratibu wakati
wa mchakato wa uteuzi wa mgombea wa urais uliofanyika Julai ambao Dk
John Magufuli alichaguliwa.
“Nimefanya makusudi kujitoa wakati huu kwa sababu hata Nyerere mwenye
angekuwapo hai leo hii angefanya uamuzi kama niliofanya. Hata yeye
alikuwa ameshachoshwa na chama chake kwa uvunjaji wa kanuni, taratibu na
katiba na alikwishaona kuwa kinaanza kupitwa na wakati.”
Alisema mengine yanayojitokeza kwa sasa ndani ya CCM yanaonyesha bayana
kuwa chama hicho hakiendi na wakati na kilijisahau na kuendesha mambo
kama kipo kwenye mfumo wa chama kimoja wakati ni wa vyama vingi.
Alisema CCM ya sasa siyo ile aliyojiunga nayo akiwa chuo kikuu, ndiyo
maana amejitoa kutokana na kutekwa na watu wachache ambao humpiga vita
mtu ambaye si mwenzao.
Ijumaa, 16 Oktoba 2015
Home »
» BAADA YA KUJITOA CCM BAKOZI JUMA MWAPACHU ATOA MPYA..ADAI HATA NYERERE ANGEKUWEPO ANGEJITOA CCM
BAADA YA KUJITOA CCM BAKOZI JUMA MWAPACHU ATOA MPYA..ADAI HATA NYERERE ANGEKUWEPO ANGEJITOA CCM
Related Posts:
Rapper mwingine wa TZ aliyetunukiwa shahada ya kwanza chuo kikuu . Rapper kutokea Unity Entertainment Stereo ambaye ameachia wimbo wake uitwao ‘Wako’ aliomshirikisha muimbaji wa Kenya,Victoria Kimani leo Des 6 ameongezewa CV yake ya Elimu baada ya kutunukiwa shahada ya ‘B… Read More
Kiongozi wa Al-Qaeda auawa Pakistan Kiongozi wa Oparesheni wa kundi la Al Qaeda auawa nchini Pakistan katika uvamizi. Kiongozi mwandamizi wa kundi la wanamgambo wa Al Qaeda anayeshukiwa kupanga kulipuwa treni mijini New York na London ameuawa … Read More
EPL: Mambo yazidi kuwa magumu kwa Wenger: Matokeo ya Stoke vs Arsenal Wakati akiwa kwenye shinikizo la kutakiwa kutimuliwa, mambo yamezidi kuwa magumu kwa kocha mkongwe zaidi kwenye ligi kuu ya England Arsene Wenger. Akiiongoza timu kwenda mpaka kwenye dimba la Brittania kucheza dhidi ya … Read More
TAKWIMU MBAYA KWA ARSENAL. Hali ndani ya klabu ya Arsenal imezidi kuwa mbaya baada ya mashabikiw a klabu hiyo kuendelea kushinikiza kuondoka kwa kocha wao Arsene Wenger . Shinikizo hilo liliongezeka mwishoni wa wiki iliyopita wakati Arsenal ilipof… Read More
Taarifa nyingine kutoka Ikulu kuhusu Rais Kikwete leo Desemba 07 Tulisikia kwamba baada ya kufanyiwa upasuaji Marekani, Rais Kikwete alipewa masharti kadhaa na madaktari waliomfanyia upasuaji juu ya utaratibu wa kufanya katika kipindi cha miezi mitatu, ambapo moja ya masharti al… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni