Siku moja baada ya kutangaza kujitoa CCM, kada mkongwe wa chama hicho,
Balozi Juma Mwapachu amesema uamuzi alioufanya ni sahihi ambao hata Baba
wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere angekuwa hai angeufanya kwa sasa.
Balozi Mwapachu alieleza hayo jana katika mahojiano maalumu na kuongeza
kuwa chama chake cha zamani kimepoteza mwelekeo kwa kuwa kinara wa
kuvunja katiba na taratibu kitendo ambacho Nyerere alikichukia katika
maisha yake.
Alisema anafahamu fika kuna watu watakosoa uamuzi wake huo lakini
hatababaishwa na maneno yao na atasimamia msimamo wake huo huku akieleza
kuwa anajisikia amani kujitoa katika siku ya kumbukumbu ya miaka 16 ya
kifo cha Nyerere.
Mwapachu alitangaza kujitoa CCM juzi akisema kilivunja taratibu wakati
wa mchakato wa uteuzi wa mgombea wa urais uliofanyika Julai ambao Dk
John Magufuli alichaguliwa.
“Nimefanya makusudi kujitoa wakati huu kwa sababu hata Nyerere mwenye
angekuwapo hai leo hii angefanya uamuzi kama niliofanya. Hata yeye
alikuwa ameshachoshwa na chama chake kwa uvunjaji wa kanuni, taratibu na
katiba na alikwishaona kuwa kinaanza kupitwa na wakati.”
Alisema mengine yanayojitokeza kwa sasa ndani ya CCM yanaonyesha bayana
kuwa chama hicho hakiendi na wakati na kilijisahau na kuendesha mambo
kama kipo kwenye mfumo wa chama kimoja wakati ni wa vyama vingi.
Alisema CCM ya sasa siyo ile aliyojiunga nayo akiwa chuo kikuu, ndiyo
maana amejitoa kutokana na kutekwa na watu wachache ambao humpiga vita
mtu ambaye si mwenzao.
Ijumaa, 16 Oktoba 2015
Home »
» BAADA YA KUJITOA CCM BAKOZI JUMA MWAPACHU ATOA MPYA..ADAI HATA NYERERE ANGEKUWEPO ANGEJITOA CCM
BAADA YA KUJITOA CCM BAKOZI JUMA MWAPACHU ATOA MPYA..ADAI HATA NYERERE ANGEKUWEPO ANGEJITOA CCM
Related Posts:
FIESTA YARUDISHA PENZI LA SHILOLE NA NUH MZIWANDA Wapenda Kunyapia nyapia Udaku wa Mastaa wa Bongo wameachwa njia panda baada ya mastaa Nuh Mziwanda na Shilole kuanza tena kuwa karibu kwa kupostiana kwenye page zao za mitandaoni, Wawili hao ambao siku za njuma wali… Read More
RUBBY ATANGAZA KUJISIMAMIA MWENYEWE BAADA YA KUTEMANA NA CLOUDS FM, ADAI SASA NI YEYE NA MASHABIKI WAKE Msanii wa Bongo Fleva, mwanadada Ruby ambaye amewahi kutamba na wimbo wake wa “Na Yule’ amefunguka na kusema kwa sasa amebadili uongozi wake na kujisimamia yeye kwani anataka kusimama yeye pamoja na mashabiki zake.R… Read More
SAKATA LA REDIO KUFUNGWA MAGIC FM YATAKIWA KUOMBA RADHI SIKU TATU MFULULIZO, REDIO 5 ZAFUNGIWA MIEZI August 29 2016 Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Nape Nnauye alitangaza kuvifungia vituo viwili vya radio kwa muda usiojulikana ambavyo ni Magic Fm ya Dar es salaam na Radio 5 ya Arusha kwa makosa ya kut… Read More
ZOMBE AACHIWA HURU, MSHIRIKA WAKE AHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA Mahakama ya Rufaa imemhukumu aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni, Christopher Bageni kunyongwa hadi kufa katika kesi ya vifo vya wafanyabiashara wa madini iliyokuwa ikimkabili yeye pamoja na aliyekuwa Mk… Read More
SERIKALI YAANZA MAZUNGUMZO YA KUWAOKOA MADEREVA 12 WALIOTEKWA CONGO Serikali imeingilia kati na kuanza mazungumzo ya kuwaokoa madereva 12 wa malori kutoka Tanzania waliotekwa nchini Kongo (DRC) na kundi la waasi wa Mai Mai.loritanzaniaWaasi hao mbali na kuwateka madereva hao wametoa saa 24… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni