Chama
Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeahidi kumshughulikia Bungeni,
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kikidai kuwa bado
hajasafishwa kwenye kashfa ya akaunti ya Escrow.
Ahadi
hiyo ilitolewa juzi na Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema Taifa, John Mnyika
katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la
Handeni, akimnadi Daudi Lusewa.
Alisema
baadhi ya mawaziri, akiwamo Muhongo, bado hawajasafishwa na tuhuma za
rushwa zilizosababisha wajiuzulu hivyo wajiandae kwani wabunge wa chama
hicho wamejiandaa kumwangusha.
Mnyika
alisema amemshangaa kuona Rais John Magufuli akimteua Muhongo kwenye
Wizara ile ile alikopatia kashfa, iliyosababisha Rais mstaafu Jakaya
Kikwete kumtema kwenye Baraza la Mawaziri.
“Hatukubaliani
na uteuzi wa Profesa Muhongo na namhakikishia bungeni patachimbika,”
alisema Mnyika ambaye ni Mbunge wa Kibamba, Dar es salaam.
“Hoja yetu ya kwanza tutakapoingia bungeni tu itakuwa kushinikiza Waziri huyu ajiuzulu maana bado hajasafishwa,” alisema Mnyika.
Jumatatu, 14 Desemba 2015
Home »
» Chadema Bado Hawajakubali Yaishe...Waapa Kumshughulikia Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo Bungeni
Chadema Bado Hawajakubali Yaishe...Waapa Kumshughulikia Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo Bungeni
Related Posts:
Polisi yaongea kwanini Diamond Platnumz hakufikishwa Mahakamani kama wale wa Singida Mohamed Mpinga ni Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani Tanzania na amekubali kukaa kwenye Interview na Ayo kujibu baada ya watu ku-comment kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuona Diamond amepost picha akiwa… Read More
Kudadadeki..Hivi Ndivyo Mbowe Alivyofanikiwa Kuwatoroka Polisi Mchana Kweupe Wakati Wakimtafuta..!!! Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam, limemtaka Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kujisalimisha Polisi mara moja kwa ajili ya Mahojiano yanayohusu vita vya dawa za kulevya baada ya ju… Read More
Makonda Hakukosea Kumtaja Wema Sepetu - Martin Kadinda Meneja wa zamani wa Wema Sepetu, Martin Kadinda amedai Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda hakukosea kumtaja Wema Sepetu kwenye list yake ya watuhumiwa wa biashara haramu ya madawa ya kulevya kutokana na aina ya… Read More
Mbeya : Mama Afukua Kaburi la Mwanae,Kisa Kamili Hiki Hapa...!!! Katika hali isiyo ya kawaida mama mmoja mwenyeji wa mkoa huu wa mbeya mji mdogo wa mbalizi, usiku wa kuamkia leo alienda kaburini alikokua kafukiwa mwanae aliyefariki dunia Siku ya jumatatu na kuzikwa jumanne ya wiki … Read More
Ripoti ya Ugunduzi Mpya wa Bara la 8 Duniani Wanasayansi wafahamisha kuwa bara la 8 lawezekana kuwa lipo chini ya bahari ya Pasifiki. Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa katika jarida la Marekani la 'Geological Society of America' ni kwamba bara hilo lim… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni