Chama
Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeahidi kumshughulikia Bungeni,
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kikidai kuwa bado
hajasafishwa kwenye kashfa ya akaunti ya Escrow.
Ahadi
hiyo ilitolewa juzi na Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema Taifa, John Mnyika
katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la
Handeni, akimnadi Daudi Lusewa.
Alisema
baadhi ya mawaziri, akiwamo Muhongo, bado hawajasafishwa na tuhuma za
rushwa zilizosababisha wajiuzulu hivyo wajiandae kwani wabunge wa chama
hicho wamejiandaa kumwangusha.
Mnyika
alisema amemshangaa kuona Rais John Magufuli akimteua Muhongo kwenye
Wizara ile ile alikopatia kashfa, iliyosababisha Rais mstaafu Jakaya
Kikwete kumtema kwenye Baraza la Mawaziri.
“Hatukubaliani
na uteuzi wa Profesa Muhongo na namhakikishia bungeni patachimbika,”
alisema Mnyika ambaye ni Mbunge wa Kibamba, Dar es salaam.
“Hoja yetu ya kwanza tutakapoingia bungeni tu itakuwa kushinikiza Waziri huyu ajiuzulu maana bado hajasafishwa,” alisema Mnyika.
Jumatatu, 14 Desemba 2015
Home »
» Chadema Bado Hawajakubali Yaishe...Waapa Kumshughulikia Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo Bungeni
Chadema Bado Hawajakubali Yaishe...Waapa Kumshughulikia Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo Bungeni
Related Posts:
Duh..Kijana wa Kiume Akamatwa Akimfanyia Mtihani wa Chuo Mpenzi Wake wa Kike..!!! Imetokea huko Zimbabwe,wote wamekamatwa wapo polisi kijana wa kiume alidai aliamua kumsaidia mpenzi wake maana amerudia mara nne anafeli tu. … Read More
Jinsi ya Kuishi na Mwanamke Asikuloge au Kukupa Limbwata..!!! Nipo tena kwa Mara nyingine katika kubadilishana uzoefu juu ya mambo mbalimbali yanayohusu mahusiano,kuna jambo limekuwa liki… Read More
Mkurugenzi wa Zamani FBI Amlipua Trump..!!! Aliyekuwa Mkuu wa Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI), James Comey ameishtumu Ikulu ya Marekani kwa kumharibia jina na kusema uongo kuh… Read More
Wema Sepetu Amzimikia Rayvanny Amtabiria Makubwa Tuzo za BET RayVanny ni msanii pekee kutoka Tanzania na Afrika Mashariki ambaye anatuwakilisha kwenye tuzo za BET zitakazofanyika Marekani baadaye mwezi huu akiwania Viewers Choice Awards ama (Pendekezo la Mashabiki ama watazamaji) hu… Read More
Kamanda wa Pwani Afafanua Mauaji ya Watu Watatu..!!! Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga amesema kwa taarifa alizonazo, watu wawili wamepigwa risasi katika kijiji cha Nyamisati, Kibiti, kisha waliofanya uhalifu huo kuwachukua majeruhi na kuondoka nao. Awali t… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni