Jumatatu, 14 Desemba 2015

Diamond Platnumz na Zari Washinda Tuzo Nchini Uganda

STAA wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinumz’ pamoja na mchumba wake Zarinah Hassan ‘Zari The Bossy Lady’ wamepata Tuzo za Abryanz Style and Fashion (ASFA 2015) zilizofanyika Kampala, Uganda usiku wa kuamkia leo.Wawili hao wameibuka kidedea katika kipengele cha East Africa Most Stylish Couple.

Mbunifu wa mavazi, Martin Kadinda naye ameibuka kidedea katika tuzo hizo kwa kipengele cha Mbunifu Bora wa Mwaka huku Mwanamitindo Bora wa Mwaka ikienda kwa Mtanzania mwingine, Dax Hannz.

Mbali na hao, pia Tanzania imepata tuzo kupitia staa wa kike wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee aliyepata katika kipengele cha East Africa’s best Dressed Female Artist.
Katika sherehe hizo zilifunikwa kwa shoo kutoka kwa mkali kutoka Nigeria, Banky W akishirikiana na bidada kunako Bongo Fleva, Linah.

Related Posts:

  • Wanajeshi 9 wa Umoja wa Mataifa wauawa  Mwanajeshi wa Umoja wa Matifa mali  Ujumbe wa Umoja wa mataifa nchini Mali unasema kuwa watu waliokuwa na silaha ambao walikuwa wakitumia pikipiki wamewaua walinda amani tisa wa Umoja wa Mataifa kaskazini ma… Read More
  • HATMA YA AFCON 2015 ? Shirikisho la soka barani afrika CAF limewaondoa mashindanoni waliokuwa wenyeji wa michuano ya AFCON Morocco baada ya taifa hilo kushikilia msimamo wake wa kutokuwa tayari kuandaa michuano ya AFCON mwaka 2015 kutokana na… Read More
  • Rais Goodluck kugombea tena urais  Rais Goodluck amekuwa akikosolewa kwa mamna anavyoshughulikia swala la Boko Haram Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amethibitisha rasmi kuwa atagombea tena kiti hicho mwaka ujao. Katika sherehe ya kufana katika mji … Read More
  • Tanzania vs Uganda katika Kickboxing. Mtanzania anayefanya vizuri kwenye mchezo wa kickboxing Emmanuel Shija hivi karibuni ataipeperusha bendera ya Tanzania nchini Uganda wakati atakapopanda ulingoni kupambana na  Mganda Moses Golola katika pambano la … Read More
  • Taarifa kuhusu ajali ya moto ulioteketeza shule ya msingi. Hii sio picha halisi ya ajali ya moto huo. Moto mkubwa umeteketeza majengo ya Shule ya msingi Filbert Bayi na kisha kusambaa na kuteketeza mabweni yote ya Wanafunzi pamoja na madarasa. Mwenyekiti wa shule hiyo Filbert … Read More

0 comments:

Chapisha Maoni