Rais Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa watumishi 
waandamizi wanne wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU 
ambao walisafiri nje ya nchi licha ya Rais Magufuli kupiga marufuku 
safari za nje kwa watumishi wa umma.
Watumishi hao ni Mary Mosha, Ekwabi Mujungu, Doreen Kapwani na Rukia 
Nikitas ambao walisafiri nje ya nchi licha ya kunyimwa kibali cha safari
 kutoka kwa Rais ama Katibu Mkuu Kiongozi.
Agizo hilo la Rais Magufuli  lilitolewa jana na Balozi Mkuu Kiongozi 
Ombeni Sefue wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari.
Balozi Sefue amewataka watumishi wengine wa umma kutii agizo la Rais wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na kuonya kuwa 
atakayekiuka atachukuliwa hatua kali.







0 comments:
Chapisha Maoni