Mshauri mkuu wa ikulu ya White House kuhusu usalama wa taifa Michael
Flynn amejiuzulu kuhusiana na uhusiano wake na maafisa wa Urusi, vyombo
vya habari Marekani vinaripoti.
Bw Flynn anadaiwa kujadili vikwazo vya Marekani dhidi ya Urusi akiwa na
balozi wa Urusi kabla ya Rais Donald Trump kuingia madarakani.
Anadaiwa kuwapotosha maafisa wa utawala huo mpya kuhusu mazungumzo yake na balozi huyo.
Awali, vyombo vya habari Marekani viliripoti kwamba Wizara ya Haki
ilitahadharisha ikulu ya White House mapema kuhusu mawasiliano ya Flynn
na maafisa wa Urusi mwishoni mwa mwezi uliopita.
Walisema Bw Flynn huenda akashurutishwa kuwa kibaraka wa urusi.
Maafisa wakuu wa chama cha Democratic walikuwa wametoa wito kwa Bw Flynn kuachishwa kazi.
Mashirika ya habari ya Associated Press na Washington Post yanasema
wizara ya haki Marekani ilitahadharisha kuhusu kile ilichosema ni mambo
aliyoyasema Bw Flynn kuhusu mazungumzo yake na balozi wa Urusi.
Ni kinyume cha sheria kwa raia wa kawaida kujihusisha na shughuli za kidiplomasia Marekani.
Mazungumzo kati ya Flynn na balozi wa Urusi yanadaiwa kufanyika mwishoni
mwa mwaka jana, kabla ya Bw Flynn kuteuliwa kuhudumu katika uatawala wa
Bw Trump.
Bw Flynn, ni luteni jenerali mstaafu.
Awali alikana kuzungumza kuhusu vikwazo dhidi ya Urusi na balozi huyo,
na Makamu wa Rais Mike Pence pia alijitokeza hadharani kumtetea.
Bw Flynn baadaye aliambia maafisa wa White House kwamba kuna uwezekano yeye na balozi huyo walizungumzia vikwazo hivyo.
Gazeti la Washington Post lilisema Kaimu Mwanasheria Mkuu Sally Yates
aliambia White House kwamba mshauri wao mkuu wa usalama wa taifa
"alijiweka katika hali ya hatari" kwa kuzungumza na Warusi kabla yake
kuruhusiwa kisheria kufanya hivyo na kwamba Wizara ya Haki ilifahamu
kwamba alimpotosha Bw Pence.
Mwezi uliopita, Bi Yates alifutwa kazi na Bw Trump kwa kukataa kutetea
marufuku yake dhidi ya raia wa mataifa saba yenye Waislamu wengi
kuruhusiwa kuingia Marekani.
Jumanne, 14 Februari 2017
Home »
» Mshauri wa Rais Donald Trump Ajiuzulu
Mshauri wa Rais Donald Trump Ajiuzulu
Related Posts:
Mengi Azomewa Diamond Jubilee, Aokolewa na Membe Mzee yamemkuta leo pale kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee leo.Ameokolewa na Mh Membe ambaye amemtoa kwa gari lake(pichani).Lakini pia Mwandishi Sam Maela wa ITV leo mchana kapata mshike mshike wa kushiba pale Lumumba,ili… Read More
Bella Amfumania Kalama na Mchepuko Ambae ni Mdogo wake...Avua Pete ya Uchumba Isabelah na Wagoni wake Tukio hilo lilijiri nyumbani kwa Bella, Makumbusho jijini Dar es Salaam baada ya kurejea ghafla kutoka safari ya kimuziki kwenye kampeni za udiwani katika Mikoa ya Iringa na Morogoro. Siku ya tu… Read More
CHADEMA Wafichua Mbinu Zilizopangwa Kuvuruga Uchaguzi wa Jumapili hi Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, Reginald Munisi (kulia) akifafanua jambo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Prof. Abdallah Safari ** ZIKIWA zimebaki siku tatu kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka… Read More
Picha 16 Za MAFURIKO Ya Lowassa Huko Tanga- Jana Oktoba 21 Mgombea urais wa Chadema anayeungwa mkono na Vyama vya Ukawa, Edward Lowassa, akipunga mkono wakati akiwasili kwenye Viwanja vya Indian Ocean katika mkutano wa kampeni mjini Tanga jana Jumatano 21/10/2015 … Read More
Familia ya Mwanamuziki Diamond Yammwaga Rasmi Zari..Sababu Hizi Hapa THE game is over! Sasa ni wazi kuwa familia ya staa mkubwa wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Plutnamz’ imemtema rasmi mzazi mwenzake Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwa kile wanachodai …. “Tumec… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni