Mshauri mkuu wa ikulu ya White House kuhusu usalama wa taifa Michael
Flynn amejiuzulu kuhusiana na uhusiano wake na maafisa wa Urusi, vyombo
vya habari Marekani vinaripoti.
Bw Flynn anadaiwa kujadili vikwazo vya Marekani dhidi ya Urusi akiwa na
balozi wa Urusi kabla ya Rais Donald Trump kuingia madarakani.
Anadaiwa kuwapotosha maafisa wa utawala huo mpya kuhusu mazungumzo yake na balozi huyo.
Awali, vyombo vya habari Marekani viliripoti kwamba Wizara ya Haki
ilitahadharisha ikulu ya White House mapema kuhusu mawasiliano ya Flynn
na maafisa wa Urusi mwishoni mwa mwezi uliopita.
Walisema Bw Flynn huenda akashurutishwa kuwa kibaraka wa urusi.
Maafisa wakuu wa chama cha Democratic walikuwa wametoa wito kwa Bw Flynn kuachishwa kazi.
Mashirika ya habari ya Associated Press na Washington Post yanasema
wizara ya haki Marekani ilitahadharisha kuhusu kile ilichosema ni mambo
aliyoyasema Bw Flynn kuhusu mazungumzo yake na balozi wa Urusi.
Ni kinyume cha sheria kwa raia wa kawaida kujihusisha na shughuli za kidiplomasia Marekani.
Mazungumzo kati ya Flynn na balozi wa Urusi yanadaiwa kufanyika mwishoni
mwa mwaka jana, kabla ya Bw Flynn kuteuliwa kuhudumu katika uatawala wa
Bw Trump.
Bw Flynn, ni luteni jenerali mstaafu.
Awali alikana kuzungumza kuhusu vikwazo dhidi ya Urusi na balozi huyo,
na Makamu wa Rais Mike Pence pia alijitokeza hadharani kumtetea.
Bw Flynn baadaye aliambia maafisa wa White House kwamba kuna uwezekano yeye na balozi huyo walizungumzia vikwazo hivyo.
Gazeti la Washington Post lilisema Kaimu Mwanasheria Mkuu Sally Yates
aliambia White House kwamba mshauri wao mkuu wa usalama wa taifa
"alijiweka katika hali ya hatari" kwa kuzungumza na Warusi kabla yake
kuruhusiwa kisheria kufanya hivyo na kwamba Wizara ya Haki ilifahamu
kwamba alimpotosha Bw Pence.
Mwezi uliopita, Bi Yates alifutwa kazi na Bw Trump kwa kukataa kutetea
marufuku yake dhidi ya raia wa mataifa saba yenye Waislamu wengi
kuruhusiwa kuingia Marekani.
Jumanne, 14 Februari 2017
Home »
» Mshauri wa Rais Donald Trump Ajiuzulu
Mshauri wa Rais Donald Trump Ajiuzulu
Related Posts:
HIKI NDICHO KIASI CHA FEDHA AMBACHO KIMEKAMILISHA VIDEO YA WIMBO MPYA WA KEREWA YA SHETAMuziki wa Tanzania umeendelea kutoa ajila kwa vijana wengi ambao baadhi yao wameamua kuwekeza Sheta ni mojawapo ya vijana ambao wameamua kuwekeza katika muziki huo kwa kuthibitisha hilo nyimbo yake ya kerewa kaenda kufanyia S… Read More
Alichokisema diamond baada ya kukosa tuzo Hii ndio kauli ya diamond baada ya davido kutwaa tuzo ya BET.Amewashuku watanzania na mashabiki wake duniani kote kwa kumsapoti hadi kufika pale alipofikia ingawa hakubahatika kupata tuzo yoyote ya kimataifa kwa mwaka… Read More
UMEISIKIA HII INAYOUSU MKATABA WA YOUNG KILLER NA MENEJA WAKE MONA GANGSTAR Mkataba wa Young killer pamoja na meneja wake ambaye vilevile ni produce wake Mona Gangstar,inawezekana huko mwishoni ingawa unaisha december mwezi huu ingawa taarifa hazina huakika. … Read More
LIST YA WACHEZAJI 16 AMBAO WANAONGOZA KWA MAGORI KOMBE LA DUNIA Michuano ya kombe la dunia imefiki hatua ya 16 bora.Huku ikionekana ni michuano ambayo ina magoli mengi mpaka hatua hii magoli 150 yameingia wavuni.Mshambuliaji wa colombia JAMES RODRIGUEZ ndio anaongoza mpaka sasa … Read More
UMEICHEKI VIDEO YA KALA JEREMIAH ALIYOMSHIRIKISHA MO MUSIC IKO HAPA Inawezekana ikawa ndiyo wimbo wa kwanza kushirikishwa na msanii kubwa baada ya kuchomoza na single yake ya Basi Nenda huyu ni Mo Music ambapo Tanzania imemtambua kwa singo yake ya Basi Nenda ambayo kupitia Clouds Fm T… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni