Hali ya ulinzi imeimarishwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete 
(JKCI) alikolazwa mfanyabiashara Yusuf Manji baada ya kuugua ghafla 
akiwa polisi alikokuwa akihojiwa.
Manji aliyekuwa akihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapa 
alipelekwa hospitalini hapo juzi jioni akiwa ndani ya gari la wagonjwa 
aina ya Toyota Land Cruiser lenye nembo ya Shirika la Umoja wa Mataifa 
la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) huku gari lake aina ya Range Rover 
likifuata kwa nyuma.
Askari wenye sare na wengine wakiwa na mavazi ya kiraia nje ya wodi 
aliyolazwa mwenyekiti huyo wa klabu maarufu nchini ya Yanga walionekana 
wakiimarisha ulinzi.
Ilipofika saa 4:13 asubuhi mfanyabiashara huyo alitoka kwenye chumba hicho na kuongozwa kuelekea upande mwingine wa jengo hilo.
Akiwa amevalia nguo za wagonjwa zenye rangi ya kijani, Manji alitembea taratibu kuelekea upande aliokuwa akielekezwa.
Alipoulizwa kuhusu uwapo wa Manji hospitalini hapo, Mkurugenzi Mtendaji 
wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi alisema hawezi kuzungumzia taarifa za 
mgonjwa.
Februari 8, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitoa orodha ya
 watu 65, akiwamo Manji ambao aliwataka wafike Polisi kwa ajili ya 
mahojiano kuhusu masuala ya dawa za kulevya.
Jumanne, 14 Februari 2017
Home »
 » Ulinzi waimarishwa Taasisi ya Moyo Muhimbili Ambako Yusuf Manji amelazwa 







 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Chapisha Maoni