Hali ya ulinzi imeimarishwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete
(JKCI) alikolazwa mfanyabiashara Yusuf Manji baada ya kuugua ghafla
akiwa polisi alikokuwa akihojiwa.
Manji aliyekuwa akihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapa
alipelekwa hospitalini hapo juzi jioni akiwa ndani ya gari la wagonjwa
aina ya Toyota Land Cruiser lenye nembo ya Shirika la Umoja wa Mataifa
la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) huku gari lake aina ya Range Rover
likifuata kwa nyuma.
Askari wenye sare na wengine wakiwa na mavazi ya kiraia nje ya wodi
aliyolazwa mwenyekiti huyo wa klabu maarufu nchini ya Yanga walionekana
wakiimarisha ulinzi.
Ilipofika saa 4:13 asubuhi mfanyabiashara huyo alitoka kwenye chumba hicho na kuongozwa kuelekea upande mwingine wa jengo hilo.
Akiwa amevalia nguo za wagonjwa zenye rangi ya kijani, Manji alitembea taratibu kuelekea upande aliokuwa akielekezwa.
Alipoulizwa kuhusu uwapo wa Manji hospitalini hapo, Mkurugenzi Mtendaji
wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi alisema hawezi kuzungumzia taarifa za
mgonjwa.
Februari 8, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitoa orodha ya
watu 65, akiwamo Manji ambao aliwataka wafike Polisi kwa ajili ya
mahojiano kuhusu masuala ya dawa za kulevya.
Jumanne, 14 Februari 2017
Home »
» Ulinzi waimarishwa Taasisi ya Moyo Muhimbili Ambako Yusuf Manji amelazwa
Ulinzi waimarishwa Taasisi ya Moyo Muhimbili Ambako Yusuf Manji amelazwa
Related Posts:
MKE WA KIONGOZI IS AKAMATWA Kiongozi wa IS Abu Bakr al-Baghdadi Vikosi vya usalama nchini Lebanon vimemkamata mkewe kiongo… Read More
Hii ni kuhusu matokeo ya zoezi la upimaji wa kilevi kwa madereva wa mabasi Ubungo Lile zoezi ambalo lilianzishwa na Jeshi la Polisi Tanzania kukagua madereva wanaoendesha mabasi ya abiria kwenda mikoani kama wanatumia kilevi leo limefanyika kwa ghafla katika Kituo cha Mabasi cha Ubungo. Taarifa iliyo… Read More
BARNES:GERRAD BADO MZURI KWA LIVERPOOLSteven Gerrard bado ana kiwango cha juu kuendelea kuitumikia Liverpool Winga wa zamani wa Klabu ya Liverpool John Barnes anaamini kiungo na nahodha wa timu hiyo Steven Gerrard, bado ni mzuri vya kutosha kuendelea kuitumik… Read More
Aliyewakosoa Sasha na Malia ajiuzuluSasha na Malia walikosolewa kwa kuvalia sketi fupi mbele ya umati katika White House Mfanyakazi katika chama cha Republican nchini Marekani amejiuzulu baada ya kukosolewa kwa kuwatuhumu wanawe Rais wa Marekani Barack Obam… Read More
NI MSANII ANAEKUJA VIZURI KUTEKA SANAA YA MUZIKI TANZANIA TOKEA KILIMANJARO Ni moja kati ya wasanii waliofanya vizuri katika tasnia ya muziki wa Tanzania kwa mwaka 2014 toka Kilimanjaro.Ramjey ndo jina lake katika sanaa akiwa amemshirikisha Rita ngoma yake inakwenda kwa jina la Sijajua kosa langu a… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni