Hali ya ulinzi imeimarishwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete
(JKCI) alikolazwa mfanyabiashara Yusuf Manji baada ya kuugua ghafla
akiwa polisi alikokuwa akihojiwa.
Manji aliyekuwa akihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapa
alipelekwa hospitalini hapo juzi jioni akiwa ndani ya gari la wagonjwa
aina ya Toyota Land Cruiser lenye nembo ya Shirika la Umoja wa Mataifa
la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) huku gari lake aina ya Range Rover
likifuata kwa nyuma.
Askari wenye sare na wengine wakiwa na mavazi ya kiraia nje ya wodi
aliyolazwa mwenyekiti huyo wa klabu maarufu nchini ya Yanga walionekana
wakiimarisha ulinzi.
Ilipofika saa 4:13 asubuhi mfanyabiashara huyo alitoka kwenye chumba hicho na kuongozwa kuelekea upande mwingine wa jengo hilo.
Akiwa amevalia nguo za wagonjwa zenye rangi ya kijani, Manji alitembea taratibu kuelekea upande aliokuwa akielekezwa.
Alipoulizwa kuhusu uwapo wa Manji hospitalini hapo, Mkurugenzi Mtendaji
wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi alisema hawezi kuzungumzia taarifa za
mgonjwa.
Februari 8, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitoa orodha ya
watu 65, akiwamo Manji ambao aliwataka wafike Polisi kwa ajili ya
mahojiano kuhusu masuala ya dawa za kulevya.
Jumanne, 14 Februari 2017
Home »
» Ulinzi waimarishwa Taasisi ya Moyo Muhimbili Ambako Yusuf Manji amelazwa
Ulinzi waimarishwa Taasisi ya Moyo Muhimbili Ambako Yusuf Manji amelazwa
Related Posts:
Familia ya Mwanamuziki Diamond Yammwaga Rasmi Zari..Sababu Hizi Hapa THE game is over! Sasa ni wazi kuwa familia ya staa mkubwa wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Plutnamz’ imemtema rasmi mzazi mwenzake Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwa kile wanachodai …. “Tumec… Read More
Bella Amfumania Kalama na Mchepuko Ambae ni Mdogo wake...Avua Pete ya Uchumba Isabelah na Wagoni wake Tukio hilo lilijiri nyumbani kwa Bella, Makumbusho jijini Dar es Salaam baada ya kurejea ghafla kutoka safari ya kimuziki kwenye kampeni za udiwani katika Mikoa ya Iringa na Morogoro. Siku ya tu… Read More
Picha 16 Za MAFURIKO Ya Lowassa Huko Tanga- Jana Oktoba 21 Mgombea urais wa Chadema anayeungwa mkono na Vyama vya Ukawa, Edward Lowassa, akipunga mkono wakati akiwasili kwenye Viwanja vya Indian Ocean katika mkutano wa kampeni mjini Tanga jana Jumatano 21/10/2015 … Read More
CHADEMA Wafichua Mbinu Zilizopangwa Kuvuruga Uchaguzi wa Jumapili hi Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, Reginald Munisi (kulia) akifafanua jambo. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Prof. Abdallah Safari ** ZIKIWA zimebaki siku tatu kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka… Read More
Mengi Azomewa Diamond Jubilee, Aokolewa na Membe Mzee yamemkuta leo pale kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee leo.Ameokolewa na Mh Membe ambaye amemtoa kwa gari lake(pichani).Lakini pia Mwandishi Sam Maela wa ITV leo mchana kapata mshike mshike wa kushiba pale Lumumba,ili… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni