Hali ya ulinzi imeimarishwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete
(JKCI) alikolazwa mfanyabiashara Yusuf Manji baada ya kuugua ghafla
akiwa polisi alikokuwa akihojiwa.
Manji aliyekuwa akihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini hapa
alipelekwa hospitalini hapo juzi jioni akiwa ndani ya gari la wagonjwa
aina ya Toyota Land Cruiser lenye nembo ya Shirika la Umoja wa Mataifa
la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) huku gari lake aina ya Range Rover
likifuata kwa nyuma.
Askari wenye sare na wengine wakiwa na mavazi ya kiraia nje ya wodi
aliyolazwa mwenyekiti huyo wa klabu maarufu nchini ya Yanga walionekana
wakiimarisha ulinzi.
Ilipofika saa 4:13 asubuhi mfanyabiashara huyo alitoka kwenye chumba hicho na kuongozwa kuelekea upande mwingine wa jengo hilo.
Akiwa amevalia nguo za wagonjwa zenye rangi ya kijani, Manji alitembea taratibu kuelekea upande aliokuwa akielekezwa.
Alipoulizwa kuhusu uwapo wa Manji hospitalini hapo, Mkurugenzi Mtendaji
wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi alisema hawezi kuzungumzia taarifa za
mgonjwa.
Februari 8, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alitoa orodha ya
watu 65, akiwamo Manji ambao aliwataka wafike Polisi kwa ajili ya
mahojiano kuhusu masuala ya dawa za kulevya.
Jumanne, 14 Februari 2017
Home »
» Ulinzi waimarishwa Taasisi ya Moyo Muhimbili Ambako Yusuf Manji amelazwa
Ulinzi waimarishwa Taasisi ya Moyo Muhimbili Ambako Yusuf Manji amelazwa
Related Posts:
Dar Mpya ya Makonda: Makonda Aitaka Takukuru Kuchunguza Madai ya Ufisadi katika Mradi wa Nyumba ‘Avic Town’ Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amenusa ufisadi katika mradi wa ujenzi wa nyumba za Avic ‘Avic Town’ na kuitaka taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kuuchunguza mradi huo uliopo Kigambo… Read More
Michirizi Inayoonekana Kwenye Miili ya Akina Dada Inaashiria Nini? Hivi Ile michirizi inayoonekana kwa baadhi ya kinadada nyuma ya goti wakiwa wamevaa sketi fupi huwa ni ishara ya utamu wao kama Mwana FA alivyoimba "Michirizi ya utamu nyuma ya goti mimi hoi na moyo hai si… Read More
Wasira: Uzee Haunizuii Kudai Haki Yangu Waziri wa muda mrefu na mbunge wa zamani wa Bunda, Steven Wasira amewajibu wanaodai kwamba amelazimika kustaafu siasa baada ya mpinzani wake, Ester Bulaya kuwashinda wapigakura wanne waliokuwa wakipinga ushindi w… Read More
Lady Jay Dee Afunga Ndoa Tena..Apost Picha Akiwa Honey Moon Msanii nguli na namba moja nchini kwa upande wa kina dada binti machozi, komamdo, anaconda, lady jay dee amefunga ndoa weekend hii kupitia mtandao wa I.G amepost baadhi ya picha akila honey moon uko Zanzibar … Read More
Model Calisah Afunguka Baada ya Kusambaa Kwa Video yake Akimla ‘Denda’ Wema Sepetu Weekend hii katika mitandao ya kijamii kumesambaa video inayomuonyesha malkia wa filamu nchini Wema Sepetu akiliwa denda na model Calisah. Wawili hao ambao walitumia nguvu nyingi kufanya siri mahusiano yao, wam… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni