Uongozi wa Uchumi Supermarket umetangaza kufunga shughuli zake katika
maduka yake yaliyopo Tanzania na Uganda ili kutoa nafasi ya kuzuia
mtikisiko wa kifedha unaoikumba kampuni hiyo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Uchumi, Dk Julius Kipng'etich, amesema Bodi
imeamua kufunga vitengo vya kikanda ili kuimarisha shughuli zake nchini
Kenya baada ya kupata hasara katika maduka yake ya Uganda na Tanzania.
"Maduka yetu ya Uganda na Tanzania huchangia asilimia 25 tu ya gharama
za uendeshaji. Matawi hayo mawili hayajapata faida yoyote kwa zaidi ya
miaka mitano iliyopita jambo linaloyumbisha shughuli zetu," amesema Dk
Julius
"Tuna uhakika kwamba tunaweza kuigeuza Uchumi kwa kulenga asilimia 95 ya
biashara ambazo zinaleta fedha kwa wanahisa ambao wana matumaini kwamba
tutafanikisha hili ndani ya muda mfupi," ameongeza Dk Kipng'etich.
Kwa upande wa Tanzania, juzi wafanyakazi zaidi ya 400 waligoma kwa
kujifungia ndani ya ofisi zao kwa zaidi ya saa 20 wakitaka kujua hatma
yao kwenye makao makuu ya duka hilo yaliyopo katika jengo la Quality
Center jijini Dar es salaam.
Alhamisi, 15 Oktoba 2015
Home »
» MADUKA YA UCHUMI SUPERMARKET YAFUNGWA TANZANIA NA UGANDA
MADUKA YA UCHUMI SUPERMARKET YAFUNGWA TANZANIA NA UGANDA
Related Posts:
Rihanna:NINA HAMU YA KUFANYA MAPENZI LAKINI.......(PICHA) Rihanna anasema yeye ni kama wanawake wengine kiasi cha kuwa na hamu ya kufanya mapenzi na kwamba hajavunja amri ya sita kwa muda mrefu sasa. rihanna-cover Akiongea kwenye jarida la Vanity Fair, Rihanna alisema hawezi tu… Read More
MADUKA YA UCHUMI SUPERMARKET YAFUNGWA TANZANIA NA UGANDA Uongozi wa Uchumi Supermarket umetangaza kufunga shughuli zake katika maduka yake yaliyopo Tanzania na Uganda ili kutoa nafasi ya kuzuia mtikisiko wa kifedha unaoikumba kampuni hiyo. Ofisa Mtendaji Mkuu wa Uchumi, Dk Jul… Read More
MWANASIASA MKONGWE MZINDAKAYA AFUNGUKA MAKUBWA KUHUSU CCM NA WALIOHAMA MWANASIASA mkongwe nchini, Chrisant Mzindakaya amewataka viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wagombea wao wa nafasi mbalimbali, wasigombane na waliohama chama hicho kwa kusisitiza kwamba wakifanya hivyo, watakuwa… Read More
DR MTIKILA ALIUAWA KABLA YA AJALI DP MAPYAA! Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrati (DP), Abdul Juma Mluya ameibuka na kusema mazingira ya kifo cha aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Mchungaji Christopher Mtikila yamejaa utata huku akiweka wazi kwamb… Read More
KILA KITU AANIKA:HATIMAYE AGNESS MASOGANGE AFUNGUKIA PENZI LA DAVIDO VIDEO Queen mwenye umbo tata Bongo, Agness Jerald ‘Masogange’ alifungukia penzi lake na staa wa muziki kutoka Nigeria, Davido. Akizungumza na Amani Masogange alisema kuwa kuna uvumi unaovumishwa na baadhi ya watu kwamba a… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni