Uongozi wa Uchumi Supermarket umetangaza kufunga shughuli zake katika
maduka yake yaliyopo Tanzania na Uganda ili kutoa nafasi ya kuzuia
mtikisiko wa kifedha unaoikumba kampuni hiyo.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Uchumi, Dk Julius Kipng'etich, amesema Bodi
imeamua kufunga vitengo vya kikanda ili kuimarisha shughuli zake nchini
Kenya baada ya kupata hasara katika maduka yake ya Uganda na Tanzania.
"Maduka yetu ya Uganda na Tanzania huchangia asilimia 25 tu ya gharama
za uendeshaji. Matawi hayo mawili hayajapata faida yoyote kwa zaidi ya
miaka mitano iliyopita jambo linaloyumbisha shughuli zetu," amesema Dk
Julius
"Tuna uhakika kwamba tunaweza kuigeuza Uchumi kwa kulenga asilimia 95 ya
biashara ambazo zinaleta fedha kwa wanahisa ambao wana matumaini kwamba
tutafanikisha hili ndani ya muda mfupi," ameongeza Dk Kipng'etich.
Kwa upande wa Tanzania, juzi wafanyakazi zaidi ya 400 waligoma kwa
kujifungia ndani ya ofisi zao kwa zaidi ya saa 20 wakitaka kujua hatma
yao kwenye makao makuu ya duka hilo yaliyopo katika jengo la Quality
Center jijini Dar es salaam.
Alhamisi, 15 Oktoba 2015
Home »
» MADUKA YA UCHUMI SUPERMARKET YAFUNGWA TANZANIA NA UGANDA
MADUKA YA UCHUMI SUPERMARKET YAFUNGWA TANZANIA NA UGANDA
Related Posts:
Kama ulisikia au kusoma kwamba Mama Diamond na Wema hawaelewani. Najua kuna stori nyingine huwa zinaandikwa alafu wahusika wakuu wanakuja kuziongelea baadae kwa kushangaa kilichoandikwa ambacho mara nyingi kinakua sio cha kweli. Stori ya Wema kutopatana na ‘mama mkwe’ yaani Mama mzaz… Read More
Kiiza, Okwi, Twite, Niyonzima, nani kumpisha mbrazil Genilson Santos ‘Jaja’ Yanga? Kuwasili kwa wabrazil wawili katika klabu ya Yanga kumeweka rehani ajira za wachezaji Emmanuel Okwi, Hamis Kiiza, Mbuyu Twite na Haruna Niyonzima kwasababu mmoja wao inabidi atemwe ili timu hiyo iweze kutimiza masharti … Read More
Magazeti ya leo July 24 2014 . Kama kawaida youngluvega.blogspot.com inakupa vichwa vya habari vya magazeti yote ya kila siku. Leo pia kuna headline mpya kwenye magazeti mbalimbali. Chukua muda wako kupitia kila kilichoandikwa kwenye kurasa za mb… Read More
Hospitali ya Muhimbili imesemaje kuhusu mabaki ya binaadamu Tegeta?Jeshi la Polisi linawahoji watu nane wakiwemo Madaktari wa chuo cha kitabibu cha IMTU kwa madai ya kutupa mabaki ya masalia ya binadamu katika msitu mdogo uliopo eneo la Mpiji kata ya Mbweni wilayani Kinondoni Dar es sala… Read More
IDADI YA JEZI ALIZOUZA JAMES RODRIGUEZ NDANI YA SAA MOJA TU.Muda mfupi baada ya kujiunga na Real Madrid kwa ada ya uhamisho wa paundi millioni 63, mchezaji wa Colombia James Rodriguez ameweka rekodi katika mauzo ya jezi yake ya Real Madrid. Ripoti za Hispania zinasema Jezi zipataz… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni