MGOMBEA urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli amemmwagia
sifa lukuki, mkali wao ndani ya muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul
‘Diamond’ kutokana na ushindi wa tuzo tatu za Afrimma zilizofanyika
wikiendi iliyopita nchini Marekani
Tukio hili lilitokea katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mpilipili mkoani
Lindi baada ya staa wa Bongo Fleva, Ali Saleh Kiba kushuka jukwaani
kukamua kwenye kampeni za mgombea huyo wa urais, ndipo Magufuli alishika
kipaza sauti na kumsifia Diamond aliyeshinda tuzo za Msanii Bora wa
Kiume Afrika Mashariki, Msanii Bora wa Mwaka na Utumbuizaji Bora wa
Video.
“Ukweli nampongeza sana msanii Diamond kwa jinsi anavyojituma na
kuipeperusha vyema bendera ya taifa letu…,” alisema Magufuli huku pia
akiwapongeza Ommy Dimpoz na Vanesa Mdee walioshinda tuzo tofauti katika
kinyang’anyiro hicho.
Aidha, katika kampeni hizo Magufuli aliwaahidi wakazi wa mji huo
kuwajengea Lindi mpya ambayo itakuwa ya neema kupitia gesi inayopatikana
kwenye ukanda huo, unafuu wa vifaa vya ujenzi ikiwemo saruji ‘cement’
iliyoanza kupatikana kwa bei ya shilingi 8,000 kwenye kiwanda cha
Dangote kilichopo Mtwara, zao la korosho ambalo Magufuli alijinandi kuwa
na digrii ya zao hilo.
Alhamisi, 15 Oktoba 2015
Home »
» MGOMBEA WA URAISI CCM DR. JOHN POMBE MAGUFULI AMFAGILIA DAIMOND PLATNUMZ
MGOMBEA WA URAISI CCM DR. JOHN POMBE MAGUFULI AMFAGILIA DAIMOND PLATNUMZ
Related Posts:
UKAWA Watishia Kutoshiriki Uchaguzi Mkuu wa Jumapili CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinachoungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kimetishia kutoshiriki katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu. Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, R… Read More
Muonekano wa Gari ya Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye, Toyota Land Cruiser Baada ya Kupata Ajali Mbaya Jana Usiku Muonekano wa gari ya Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye, Toyota Land Cruiser baada ya kupata ajali mbaya jana usiku akiwa njiani kuelekea Lindi akitokea jijini Dar es Salaam. … Read More
Katibu Mwenezi wa CCM Nape Nnauye Apata Ajali Mbaya ya Gari KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye amepata ajali mbaya jana usiku akiwa njiani kuelekea Lindi akitokea jijini Dar es Salaam. Nape ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama, Lindi &… Read More
Hatimaye Mama Maria Nyerere Ampigia Kampeni Magufuli CCM tayari wameshatengeneza video ya mama Maria Nyerere akiwaomba akina mama wotewampigie kura Magufuli. Video hii iko inasambaa Whatsup. Kaongea mengi kuwa ni mchapa kazi na Mwadilifu. Swali langu kwa bibi angu mama Ma… Read More
Madai ya Kumuua Mwigizaji Kanumba LULU MICHAEL Mahakani Tena... Stori: Na Brighton Masalu MAMBO yameiva! Nyota wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ (20) yu mbioni kupanda tena Kizimba cha Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam kwa ishu yake ile ya madai y… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni