Rais John Magufuli anaongoza kura za kuwania tuzo ya ‘Forbes Africa
Person of The Year’, ambayo hutolewa kwa watu walioonyesha mchango kwa
jamii.
Huku zikiwa zimebaki siku 21 kwa mshindi wa tuzo hiyo kutangazwa, Rais
Magufuli anachuana na Rais wa Mauritius, Ameenah Gulib; Mwendesha
Mashtaka wa Afrika Kusini, Thuli Madonsela; Mwanzilishi wa Capitec Bank,
Michiel Le Roux na Taifa la Rwanda.
Mpaka jana jioni, Dk Magufuli alikuwa anaongoza kwa asilimia 75
likifuata Taifa la Rwanda na nafasi ya tatu alikuwa Madonsela wa Afrika
Kusini.
Rais Magufuli anayetimiza mwaka mmoja madarakani wiki ijayo, utendaji
wake umeonekana kuwagusa wananchi wa kipato cha chini, hasa kwa falsafa
yake ya Hapa Kazi, uwajibishaji na mikakati yake ya kubana matumizi ili
kuokoa fedha kwa kuzuia sherehe zisizo na tija.
Jumatano, 26 Oktoba 2016
Home »
» Rais Magufuli Aongoza Kura Kuwania Tuzo ya ‘Forbes Africa Person of The Year’
Rais Magufuli Aongoza Kura Kuwania Tuzo ya ‘Forbes Africa Person of The Year’
Related Posts:
WASANII NA VIONGOZI WA WCB WAALIKWA NYUMBANI KWA RAISI MSTAAFU JAKAYA KIKWETE Rais mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete Jumatano hii aliwaalika wasanii wa label ya WCB pamoja na viongozi nyumbani kwake na kula nao chakula cha mchana. JK ambaye ni mmoja kati ya marais ambaye amesupport sana wasanii … Read More
DADA WA DAIMOND ESMA PLATNUMZ AKIRI KUMPENDA SANA PETIT MAN AWAOMBA NYAKU NYAKU WASIMNYAKUE Dada wa Diamond ameamua kufunguka ya moyoni na kudai anampenda sana mume wake Petit Man ambae walitengana kwa muda kutokana na kutokuelewa hapa na pale lakini kwa sasa inaonekana wameweka mambo sawa...Ameandika haya… Read More
GAVANA BOT AFICHUA SIRI YA KILIO CHA FEDHA KUPOTEA MTAANI Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Benno Ndulu jana alitolea ufafanuzi hali ya kiuchumi nchini huku akieleza siri ya kilio kinachovuma cha fedha kupotea mtaani na nyingine zikidaiwa kufichwa.Akizungumza na waa… Read More
EDWARD LOWASSA AMPONGEZA RAISI JOHN POMBE MAGUFULI Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa amempongeza Rais Magufuli kwa kuondoa urasimu katika taasisi za serikali na kusema hiyo itasaidia kurejesha utendaji kazi kwa ufan… Read More
FAIZA ALLY AFUNGUKA KUMPENDA SUGU KUTOKA MOYONI..ADAI HAOGOPI KUCHEKWA KWA KIGEUGEU CHAKE Faiza Ally Amefunguka haya Katika ukurasa wake wa Instagram:Leo nimeamka akili yangu inawaza mapenzi tu... Mkatae mkubali mapenzi yana nafasi kubwa sana ktk maisha... Na mapenzi hayana baunsa...😅 Mimi nampenda sana… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni