THE game is over! Sasa ni wazi kuwa familia ya staa mkubwa wa muziki wa
kizazi kipya Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Plutnamz’ imemtema rasmi mzazi
mwenzake Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwa kile wanachodai ….
“Tumechoshwa na uzungu wake”, Risasi Mchanganyiko linaweza kuandika.
Chanzo kilicho karibu na familia hiyo kililiambia gazeti hili kuwa kina
taarifa kuwa mama Latiffa ‘Tiffah’ hatarejea tena nchini kutokana na
kushindwana na wanafamilia, kwani wanaendekeza uswahili, kitu ambacho
yeye hakiwezi.
“Familia ya Diamond ndiyo imemchoka, unajua yule hajazoea mambo ya
kiswahili swahili, ametofautiana nao sana na ndiyo maana hata wao
wamesema hawamtaki tena, wanahitaji mswahili mwenzao,” kilisema chanzo
hicho.
FAMILIA YA DIAMOND HII HAPA
Ili kujua ukweli wa maelezo hayo, mwandishi wetu alimtafuta mama mzazi
wa Diamond, Sanura Kassim ‘Sandra’ kupitia simu yake ya mkononi, na
alipoulizwa, alihamaki na kuanza kufoka, akidai hataki kuingiliwa mambo
yake ya ndani na kwamba kama kuna mtu anataka kujua zaidi amfuate Zari
huko kwao (South Afrika).
“Hata kama ni kweli, mimi na huyo sijui Zari wenu tumegombana wewe
yanakuhusu nini? sipendi kuingiliwa kwenye mambo ya familia yangu,
ninachojua ni kwamba hayupo hapa na maisha yanaendelea,” alisema Mama
Diamond na kukaa kimya huku simu ikiwa hewani.
Wakati simu ikiwa hewani, ghafla sauti ya kiume ilisikika na
kujitambulisha kwa jina la Anko Salum, aliyemtaka mwandishi kuachana na
habari hizo, kwani ni za ndani na zitamalizwa na wenyewe kama familia.
Wakati mwandishi wetu akiendelea kuzungumza na Anko Salum, ghafla tena
sauti nyembamba na kali masikioni ilisikika na mwanahabari wetu
akaibaini kuwa ni ya Esma, ambaye ni dada wa Diamond.
“Mbona mnatufuatilia sana jamani? Nani anafuatilia mambo yenu? Nafasi ya
Zari imefika mwisho, tunamkaribisha mwingine yeyote, kama kuna msichana
mrembo unamjua, tuletee nyumba yetu ni kubwa sana, na sisi tunaruhusiwa
kuoa hata wanawake wanne, Zari ameishia hapo, tena hatujagombana naye,
lakini tumechoshwa na uzungu wake, awamu hii tunahitaji mswahili
mwenzetu.
“Zari ameenda kwao, kulea watoto wake na kuangalia ustaarabu mwingine,
tunamtakia kila la kheri, lakini hatuna ugomvi naye kabisa,” alisema
Esma.Jitihada za kumpata Diamond hazikuzaa matunda kutokana na namba
yake ya mkononi kutokuwa hewani kila alipopigiwa, hata hivyo jitihada
zaidi zinaendelea kumtafuta.
Source:Global Publishers
Alhamisi, 22 Oktoba 2015
Home »
» Familia ya Mwanamuziki Diamond Yammwaga Rasmi Zari..Sababu Hizi Hapa
Familia ya Mwanamuziki Diamond Yammwaga Rasmi Zari..Sababu Hizi Hapa
Related Posts:
Jinsi Facebook ilivyowafanyia utafiti wa kisaikolojia watumiaji bila kuwajulisha. Mtandao wa kijamii wa Facebook umelaumiwa kwa kuwafanyia wateja wake utafiti wa kisaikolojia bila ya kuwajulisha.Shirika la habari la BBC limeripoti kuwa, nia ya utafiti huo ilikuwa kujua kama wateja wake wamebadili tabia y… Read More
Single mpya ya Madee umeipata?inaitwa Ni sheedah isikilize hapa. Kwa mfumo wa muziki wa Madee huu anauita muziki wa Kwata ambao ni muunganiko wa Kwaito na Takeu ndio unautengeneza Kwata,single ya 3 kutoka kwake baada ya Pombe Yangu,Tema mate tuwachape na hii Nisheeeda.Bonyeza play kusiki… Read More
Malalamiko ya Shilole kuhusu Dj wa Club anayetaka kumdhulumu Laptop yake. Kutoka kwa Soudy Brown kupitia You heard ya leo Shilole amelalamika juu ya mtu anayedai kumuazima laptop yake lakini anaonekana ana dalili za kumdhulumu baada ya simu zake kuwa hapokei, amemtaja kwa jina la Dj Ommy Crazy am… Read More
Jinsi Beyonce alivyobadilisha mistari ya wimbo wake jukwaani kufuatia matatizo ya ndoa yake. Wanandoa Beyonce na Jay Z wamekuwa wakipambana na uvumi kuwa sasa ndoa yao iko juu ya mawe kutokana na matatizo makubwa yanayoendelea tangu kusambaa kwa video ikimuonyesha dada wa Beyonce Solange akimshambulia Jay Z. Na s… Read More
Angalia magoli 10 bora ya kombe la dunia – Messi vs Van Persie nani katisha? Michuano ya kombe la dunia ipo kwenye hatua ya robo fainali ambayo itaanza rasmi Ijumaa hii. Michuano hii ya mwaka huu imekuwa na magoli mengi na bora katika historia ya michuano hii mikubwa kabisa katika soka.youngluvega.c… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni