CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinachoungwa mkono na Umoja
wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kimetishia kutoshiriki katika Uchaguzi
Mkuu utakaofanyika Oktoba 25, mwaka huu.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Chadema, Reginald Munisi amesema wanadhamilia
kutoshiriki katika uchaguzi huo kutokana Tume yaTaifa ya Uchaguzi (NEC)
kutokuwa na msimamo katika kazi zake.
Anasema zikiwa zimebaki siku tatu wananchi kuelekea kwenye uchaguzi mkuu
lakini NEC hadi sasa haina msimamo na kuonekana kuyapuuza madai mengi
yenye hoja yanayotolewa na Ukawa.
Akiyataja baadhi ya madai ambayo NEC imeyapuuza ni kutotoa ushirikiano
wa kufafanua juu ya upigaji kura kwa watu ambao hawakuona majina yao
kwenye daftari la kupiga kura na kutotoa sababu ya utofauti wa namba za
kupigia kura kutoka kwenye daftari na kwenye kitambulisho.
Munisi ameongeza kuwa, NEC wamepuuza kutoa ufafanuzi juu ya picha ambazo
haziitajiki katika upigaji kura, kutoa ufafanuzi juu ya listi mpya ya
wapiga kura iliyosemwa na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva,
kwamba kutakuwa na watu wa ziada ambao hawapo kwenye daftari, Je,
wanatoka wapi na wapo wangapi? Amehoji.
“Kwa mtindo huu ambao NEC inaenda nao wa kukubali watu wasiokuwa
kwenye daftari wapige kura na hata wasiokuwepo kwenye orodha wapige kura
mbona hawakutushirikisha sisi wadau wa uchaguzi? Inaweza kupelekea
uvunjifu wa amani. Hilo ndio bao la mkono ambalo lilisemwa na hatutaki
litokee,” anasema Munisi.
Munisi amesema sababu nyingine kubwa ambayo inaweza kupelekea
wasishiriki kwenye uchaguzi ni kuhusu madudu yaliyopo ndani ya daftari
la wapiga kura, ambapo hadi sasa NEC haijatoa jibu linaloeleweka juu ya
makosa ambayo yalionekana kwenye daftari.
Sababu nyingine ya kutaka kutoshiriki amesema, “Hatuna imani na
ujumlishaji wa matokeo ya kura kwa njia ya mashine zao za kujumlisha
kwani zinamapungufu mengi. Tuliomba tume itumie njia ya kawaida kwa njia
ya kalukuleta ili kila mtu alidhike lakini walidai tunawaingilia kazi
zake. Sisi hatutakubali,” amesema Munisi.
Kwa mujibu wa Munisi amesema, hadi sasa bado wanaendelea na uchunguzi
kwenye madaftari ya wapiga kura ambapo amesema wameshakagua katika mikoa
tisa na kubaini matatizo mengi zaidi yakiwemo ya picha hewa, picha za
watu wawili na majina ya kiume kwenye picha za kike.
“Hapo hatujafanya katika majimbo yote tulifanya baadhi. Bado
tunaendelea na uchunguzi hadi kesho, tukiona makosa yanazidi kiwango cha
kufanya uchaguzi usiende vizuri basi tunaiomba NEC ipeleke uchaguzi
mbele,” amesema Munisi.
Aidha, ameitaka NEC kutoa orodha maalumu ya vituo vya kupigia kura kwani
hadi sasa Ukawa bado hawajajua idadi kamili ya vituo hivyo wanashindwa
kuwaapisha mawakala kwa idadi ya vituo kubadilishwa kila siku.
Alhamisi, 22 Oktoba 2015
Home »
» UKAWA Watishia Kutoshiriki Uchaguzi Mkuu wa Jumapili
UKAWA Watishia Kutoshiriki Uchaguzi Mkuu wa Jumapili
Related Posts:
WANACHAMA 100 WA BOKO HARAM WAUAWA jeshi la Nigeria Jeshi la Nigeria linasema kuwa limewaua zaidi ya wanamgambo 100 wa kundi la Boko Haram kufuatia shambulizi la wapiganaji hao siku ya ijumaa kazkazini mashariki mwa jimbo la Borno. Vikosi vya ser… Read More
MAYWEATHER AMCHAPA TENA MAIDANA Floyd Mayweather (kushoto) akimtupia konde mpinzani wake Marcos Maidana. Maidana akijibu mashambulizi wakati wa pambano hilo. Mayweather akimshambulia mpinzani wake.… Read More
Habari njema! Fastjet tena kwenye headlines!! wameanza kwenda Uganda. Shirika la ndege la Fastjet limepata sifa kubwa nchini Tanzania kutokana na kusafirisha kwake abiria na kuanza kuiunganisha Afrika kwa kasi ambapo baada ya kuanzisha safari za nyumbani kati ya Mwanza – Dar, Kilimanjaro – D… Read More
Sentensi 4 kwanini maandamano ya CHADEMA Dodoma kesho yamezuiliwa. Polisi Dodoma wametangaza kuyazuia maandamano ya chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA yaliyokua yamepangwa kufanyika Alhamisi ya tarehe 18/09/2014 ambapo wametaka Wananchi wayapuuze. Kaimu Kamanda wa Polisi Mk… Read More
UGANDA YAHARIBU SHAMBULIZI LA KIGAIDI Vikosi vya usalama nchini Uganda Maafisa wa polisi nchini Uganda wameimarisha usalama katika maeneo mengi ya uma katika mji mkuu wa Kampala kufuatia kukamatwa kwa washukiwa kadhaa wa makundi ya kigaidi na vil… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni