KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye
amepata ajali mbaya jana usiku akiwa njiani kuelekea Lindi akitokea
jijini Dar es Salaam.
Nape ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama, Lindi alipata
ajali hiyo baada ya tairi la mbele la gari aliyokuwa akiendesha aina ya
Toyota Land Cruiser kupasuka na kupinduka mara kadhaa katika eneo la
Nyangao mkoani Lindi.
Katika gari hilo, Nape alikuwa peke yake na ndiye alikuwa akiendesha
gari hilo ambapo amepata majeraha madogo ila anaendelea vizuri.
Akizungumza na mtandao huu, Nape amesema: “Namshukuru Mungu nimetoka
salama na nawaomba wananchi wasiwe na hofu japo ajali ilikuwa mbaya
maana gari lilipinduka mara kadhaa, nimepata majeraha madogomadogo na
michubuko ila ni mzima.
Gari limeharibika vibaya ila ninachoshukuru nilikuwa nimefunga mkanda na ‘air bag’ nazo zimenisaidia.”
Kabla ya ajali hiyo, Nape alikuwa jijini Dar es Salaam ambapo aliungana
na mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Pombe Magufuli aliyekuwa na
mikutano kadhaa ya kampeni katika jiji la Dar na baada ya shughuli hiyo
alikuwa akirejea Lindi kuendelea na kampeni kwenye jimbo lake la Mtama.
Source:GPL
Alhamisi, 22 Oktoba 2015
Home »
» Katibu Mwenezi wa CCM Nape Nnauye Apata Ajali Mbaya ya Gari
Katibu Mwenezi wa CCM Nape Nnauye Apata Ajali Mbaya ya Gari
Related Posts:
Hivi Ndivyo Uzuri wa House Girl Ulivyomponza Mke wa MTU Mpaka Akaambukizwa Ukimwi Inasikitisha sana. Fuatilia mkasa huu mwanzo mwisho.... Mke alimhisi mmewe kuwa anatembea na housegirl wao kutokana na ukweli kuwa, housegirl alikuwa mzuri mno kimuonekano, kiumbo na kwa sura. Alifikiri kumfukuza ila m… Read More
Baada ya Sekeseke la Madawa ya Kulevya Kutulia,TID Aamua Kumtaja Tena Diamond..!!! Kwa sasa msanii TID Mnyama anahakikisha anarudisha makali yake ya zamani kwenye muziki. Muimbaji huyo amewaahidi mashabiki wake kufanya kazi na Diamond hivi karibuni. Akiongea kwenye kipindi cha XXL, kupitia Clouds … Read More
Binadamu Kuanza Kuwekewa Moyo wa Plastiki,Soma Hapa Kujua Utakavyofanya Kazi...!!! NCHINI Marekani kila baada ya dakika 10 mtu mmoja huwekwa kwenye foleni ya watu wanaosubiri kuwekewa moyo mpya ili kuweza kuendelea kuishi. Hali hii hoto… Read More
Mwanamke Aelezea Jinsi Askari Walivyombaka Msumbiji Wakati Serikali ikiahidi kufanya uchunguzi wa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika kutimua Watanzania nchini Msumbiji, mwanamke mmoja amesema alibakwa na askari watatu kabla ya kuwekwa mahabausu ambako ali… Read More
Makubwa Haya..Ray C Afunguka Kumpenda Rayvanny,Adai Anatamani...!!! Msanii mkongwe wa Bongo Fleva mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni, Ray C amedai kuwa anamkubali zaidi Rayvanny kutoka lebo ya WCB. Ray C amesema kuwa amesikia msanii huyo amewaandikia wasanii wengi nyimbo hivyo n… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni