KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye
amepata ajali mbaya jana usiku akiwa njiani kuelekea Lindi akitokea
jijini Dar es Salaam.
Nape ambaye pia ni mgombea Ubunge wa Jimbo la Mtama, Lindi alipata
ajali hiyo baada ya tairi la mbele la gari aliyokuwa akiendesha aina ya
Toyota Land Cruiser kupasuka na kupinduka mara kadhaa katika eneo la
Nyangao mkoani Lindi.
Katika gari hilo, Nape alikuwa peke yake na ndiye alikuwa akiendesha
gari hilo ambapo amepata majeraha madogo ila anaendelea vizuri.
Akizungumza na mtandao huu, Nape amesema: “Namshukuru Mungu nimetoka
salama na nawaomba wananchi wasiwe na hofu japo ajali ilikuwa mbaya
maana gari lilipinduka mara kadhaa, nimepata majeraha madogomadogo na
michubuko ila ni mzima.
Gari limeharibika vibaya ila ninachoshukuru nilikuwa nimefunga mkanda na ‘air bag’ nazo zimenisaidia.”
Kabla ya ajali hiyo, Nape alikuwa jijini Dar es Salaam ambapo aliungana
na mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Pombe Magufuli aliyekuwa na
mikutano kadhaa ya kampeni katika jiji la Dar na baada ya shughuli hiyo
alikuwa akirejea Lindi kuendelea na kampeni kwenye jimbo lake la Mtama.
Source:GPL
Alhamisi, 22 Oktoba 2015
Home »
» Katibu Mwenezi wa CCM Nape Nnauye Apata Ajali Mbaya ya Gari
Katibu Mwenezi wa CCM Nape Nnauye Apata Ajali Mbaya ya Gari
Related Posts:
Linah amerudi Dar! ameongea kuhusu kolabo na Uhuru na Dj Malvado South Africa Katikati ya June 2014 Linah alizungumza na Young luvega.com akiwa South Africa na kuthibitisha kwamba kilichompeleka huko na kumfanya akae kwa zaidi ya siku 20 ni kazi ya muziki.Miongoni mwa alivyokua anavifata ni kufanya … Read More
Nakualika kutazama video mpya ya Ben Pol – Unanichora. Hii ni video ambayo imeongozwa na mshindi wa tuzo ya Muongozaji[Director] anayependwa Nisher kutoka Arusha,ni video ya pili kutoka kwa Ben Pol baada ya kufanya nae video ya Jikubali,baada ya kuangalia unaweza kuandika choch… Read More
Pale girlfriend wa Chris Brown alipokutana na @DiamondPlatnumz na kumuhoji kwenye red carpet Karrueche Tran mrembo ambae ni mpenzi wa mwimbaji staa wa dunia Chris Brown alihusika kama mtangazaji na kuhoji watu mbalimbali waliohudhuria tuzo za BET 2014 ambazo Mtanzania Diamond Platnumz alichaguliwa kushiriki kama … Read More
Ebana umekiona kipande cha video ya Diamond ft Iyanya..kipo hapa Hii h Diamond ameshafanya kazi nyingi ambazo bado hazijatoka, moja kati ya hizo ni audio na video yake na Iyanya.apa ni teaser ya video ya wimbo wa Bum bum akiwa na Iyanya. Sekunde 15 zinatosha kuangalia teaser yote, e… Read More
Hizi ndizo siku zilizobaki hadi wimbo mpya wa @Shaa_tz utoke. Kama bado haujaona picha na video za behind the scene wakati Shaa anarekodi video ya wimbo huu basi utaziona hapa. Wimbo unaitwa Subira ukiwa ni wa pili tangu aanza kufanya kazi na Mkubwa na wanae baada ya kutoa Sugua gaga.… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni