Kwa
 wanaofatilia siasa za kenya kulikua na skendo iliyokua inamuhusu waziri
 wa uhuru Anne Waiguru, huyu Anne Waiguru alikua ni waziri mtu mkubwa na
 maarufu serikalini.
Zimepotea
 795 milion kshs ambazo ni kama 16 billion tz shs amewajibishwa na 
nyumbani kwake kumepekuliwa na maofisa wa kupambana na rushwa na kukuta 
mamilioni ya pesa kwenye mabunda, soon atafunguliwa mashtaka na 
kufungwa.
Juzi
 hapa Tanzania ufisadi wa escrow umetu cost zaidi 300 billions lakini 
hakuna hata mmoja aliyepekuliwa na wote wamerudi kua wabunge.
Tunatakiwa
 kuiga wakenya, sio tunatimua maofisa wa tra na muhimbili alafu tunaanza
 kujiisifu sana bado tuna safari ndefu kwenye hii vita dhidi ya ufisadi.
Sina nia ya kubeza anachofanya Magufuli, nampongeza ila tunapaswa kushinikiza yafanyike zaidi ya hapa na tumuunge mkono.
Kenya wana upinzani imara ndio maana kukitokea ubadhirifu kidogo tu wanaibana serikali hadi inawachukulia hatua wahusika.
Tusiwabeze
 wapinzani wa serikali tuwasapoti maana wao ndio wanaweza kuibana 
serikali kwa niaba yetu panapofanyika madudu kama haya







 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Chapisha Maoni