Serikali ya Ujerumani imeeleza kufurahishwa na kasi ya kupambana na
rushwa na ufisadi ya Rais John Magufuli na kuahidi kumpa ushirikiano
katika masuala ya maendeleo.
Ujerumani inakuwa nchi ya kwanza ya kigeni kuvutiwa na kasi ya Rais
Magufuli ambaye ameonekana kuelekeza nguvu katika si tu kupambana na
maovu hayo tangu aapishwe Novemba 5, bali pia kuchochea maendeleo ya
watu wenye kipato cha chini.
Aidha, Ujerumani imesema inasubiri kuona vipaumbele vya maendeleo
vitakavyoainishwa na serikali ya Rais Magufuli ili iweze kuisaidia
utekelezaji.
Pongezi hizo zilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Afrika, Wizara ya Mambo ya Nje ya Ujerumani, Georg Schmidt.
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ziara yake ya siku tano hapa
nchini, Schmidt alisema katika kipindi cha mwezi mmoja tu, Dk. Magufuli
ameweza kushughulikia masuala muhimu ya kijamii ikiwamo kuboresha huduma
za afya na kuwashughulikia wakwepa kodi.
Kasi ya Rais Magufuli, alisema, itasaidia kuokoa fedha nyingi ambazo
zitakapokusanywa zitachangia miradi mbalimbali ya maendeleo kama
alivyofanya tayari kwenye afya na elimu.
Mkurugenzi huyo alisema ziara yake nchini ilikuwa na lengo la kuangalia
hali ya maendeleo nchini baada ya uchaguzi, miradi ya maendeleo
inayotekelezwa na serikali yake pamoja na kukuza ushirikiano baina ya
nchi mbili hizo.
Alisema ameshakutana na baadhi ya watendaji wa serikali, wabunge,
wanaharakati, watendaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na
kuitembelea Mahakama ya Haki za Binadamu iliyopo mjini Arusha.
Alisema pia amekuja kuangalia fursa za kibiashara nchini kwa sababu
wawekezaji wengi duniani huvutiwa kwenda kuwekeza kwenye mataifa
mbalimbali iwapo nchi hiyo ina usalama wa kutosha.
Akizungumzia suala la Zanzibar, Schmidt aliwataka wananchi kuwa na
subira wakati mazungumzo yakiendelea katika jitihada za kutatua mgogoro
huo.
“Mazungumzo yanaendelea ya usuluhishi tunasisitiza utulivu, amani na tuna imani mwafaka mzuri utafikiwa,” alisema.
Alisema kwa sasa serikali ya Ujerumani itazielekeza fedha nyingi kwa
serikali ya Tanzania ili kushughulikia wakimbizi kutoka Burundi
wanaokimbia machafuko.
“Tuna jukumu na wajibu wa kushughulikia mgogoro wa Burundi na fedha
zilizokuwa zinakwenda Burundi sasa zitaelekezwa Tanzania kwa kuwa
wanapokea wakimbizi wengi zaidi,” alisema Schmidt.
Jumapili, 6 Desemba 2015
Home »
» Ujerumani Yamsifu Rais Magufuli Kwa Kupambana na Ufisadi Kwa Vitendo.....Yaahidi Kumpa Ushirikiano
Ujerumani Yamsifu Rais Magufuli Kwa Kupambana na Ufisadi Kwa Vitendo.....Yaahidi Kumpa Ushirikiano
Related Posts:
Rumishael Shoo (Rummy) Ashikiliwa na Polisi Kwa Tuhuma za Dawa ya Kulevya Kamanda Sirro akiongea na waandishi wa habari amesema Jeshi la Polisi limefanikiwa kuwakamata wahalifu mbalimbali, silaha na magari mawili aina ya Noah yaliyokuwa yakitumika kufanya uhalifu. Miongoni mwa aliowata… Read More
Ishara Za Kujua Iwapo Umemkuna Mwanamke Wako Vizuri Kunako 6 X 6..!!! Leo acha niwape dondoo kadhaa kuhusu namna ya kujua kama umemkuna ipasavyo mwanamke wakati wa tendo la ndoa. 1.Kufinya shuka kwa nguvu au kitanda kwa nguvu wakati unampa mambo ni ishara mojawapo ya kuonye… Read More
DODOMA: Bashe, Malima na Musukuma Mbaroni Wakidaiwa Kupanga Kuhujumu Vikao Vinavyoendelea Wabunge wawili Bashe na Musukuma wamekamatwa leo asubuhi kabla ya kikao cha Kamati Kuu kuanza kutokana na kudaiwa kubeba ajenda ya "kwenda kumpinga Mwenyekiti". Kundi hili la wabunge lililokuwa na mjumbe mwingine, Adam M… Read More
P-Funk: Diamond Anapaswa Kutulia Kidogo, lasivyo Watu Watamchoka Producer mkongwe wa Bongo Records, P-Funk Majani, amesema kila siku akiendelea kusikia kuhusu Wasafi, itafika muda atawachoka. Amedai kuwa ili label hiyo iendelee kufanya vizuri kwa muda mrefu, ni lazima ibadili… Read More
Wakati Mwingine Wanasiasa Wawe Wakweli, Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa Hakuwa na Ziara Rasmi Tanzania..!!!! Naona watu wameibeba hii ya Katibu Mkuu wa UN kama "ajenda" tena,huku namuona Mtatiro akirusha makombora,na huku Mbunge Msigwa akirusha kwa upande wa pili.Vijana nao wamebeba mitandaoni kama ajenda ya kumalizia week k… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni