Kikosi cha magwiji hao maarufu kama 
`Real Madrid Legends` kitafanya ziara ya siku nne nchini kuanzia Agosti 
22 mwaka huu na kitacheza mechi moja ya kirafiki dhidi ya kikosi maalumu
 cha nyota wa Tanzania.
Akizungumza leo na waandishi wa 
habari katika hoteli ya New Afrika, jijini Dar es salaam, meneja wa 
ziara hiyo, Dennis Ssebo amesema  mbali na Vodacom, wadhamini wengine ni
 Fastjet, Tropical, Pembe Flower, Lake Gas, EFM Radio na Ladger Plaza 
Bahari Beach.
Ziara hiyo ni mwaliko wa kampuni ya 
Tanzania Sisi ni Nyumbani (TSN), chini ya mkurugenzi wake mkuu, Farough 
Baghozah na meneja wa ziara hiyo ni Dennis Ssebo.
Wachezaji wa Real Madrid waliocheza 
La Liga miaka ya nyuma, ligi ya mabingwa kombe la dunia kama vile 
Mfaransa Zinedine Zidane, Mreno Luis Madeila Figo na Mbrazil Ronaldo de 
Lima watakuwepo katika ziara hiyo.
Ssebo kabla ya mkutano wa leo, 
aliuambia mtandao huu kuwa maandalizi ya ziara hiyo yanakwenda vizuri na
 itakuwa fursa pekee kwa Watanzania kuiona Real Madrid kwa mara ya 
kwanza barani Afrika.
 “Ninaloweza Kusema ni kwamba, 
 Watanzania wakae tayari kupokea wachezaji 27 wa zamani wa timu ya Real 
Madrid na mashabiki 23  kutoka Hispania wanaokuja kuwashangilia magwiji 
wao. Kwahiyo jumla tunapokea watu 50 kutoka Hispania kwa ajili ya ziara 
hii”. Alisema Ssebo.
“Ni ziara ambayo tulifikiria itakuwa 
fupi, lakini wenzetu kumbe wameipenda nchi na wanaifahamu, kwahiyo ni 
ziara ambayo itachukua takribani siku nne”. Aliongeza.






 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Chapisha Maoni