
Moto huo ambao inaelezwa chanzo chake ni hitilafu ya umeme ilitokea wakati wanafunzi wote wako darasani.
Hakuna mtu yoyote aliyedhurika lakini mali kadhaa za wanafunzi zimeteketea. Kikosi Cha zimamoto kutoka Arusha kilifika wakati tayari mabweni hayo yameshateketea.
Mbunge wa Jimbo la Monduli Mh Edward Lowassa ametembelea shule hiyo na kuahidi kuwasafirisha wanafunzi majumbani kwao wakati utaratibu unafanywa kurejesha katika hali ya kawaida.
Gharama za kuwasafirisha wanafunzi hao ni shilingi laki Saba. Aidha Mh Lowassa amesema kiwanda Cha magodoro Cha Tanform Cha Arusha kimetoa msaada wa magodoro 100 kufuatia kadhia hiyo.
0 comments:
Chapisha Maoni