Jumapili, 12 Februari 2017

Jaji Chande Apewa Kazi Umoja wa Mataifa..!!

Jaji Mkuu mstaafu Othman Chande ameteuliwa kuongoza jopo la wataalamu watakaochunguza mazingira yaliyosababisha ajali ya ndege iliyomuua aliyekuwa katibu mkuu wa umoja huo, Dag Hammarskjold.
Uteuzi huo wa jaji mkuu mstaafu umefanywa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Antonio Guterres.
Hammarskjold alipoteza maisha katika ajali ya ndege iliyotokea Zambia mwaka 1961 wakati akitokea Congo ambayo ndiyo kwanza ilikuwa imepata uhuru.
Hammarskjold alikuwa nchini humo kwa ajili ya ujumbe wa amani.
Naibu msemaji wa UN, Farhan Haq amesema Chande ataongoza jopo hilo ambalo litakuwa na kazi kupitia taarifa zilizoandaliwa na wachunguzi waliopewa jukumu na katibu mkuu mstaafu, Ban Ki-moon.
Uchunguzi huo unafuatia azimio la Umoja wa Mataifa lililopitishwa na Baraza Kuu ambalo lilipendekezwa kufanyika uchunguzi wa kina kubaini mazingira ya ajali hiyo.
Awali, kulikuwa na ripoti kuwa Uingereza na Marekani zilikuwa zimegoma kutoa baadhi ya taarifa muhimu kuhusu tukio hilo, huku Afrika Kusini ikilalamikiwa kwa kushindwa kutoa majibu kwa baadhi ya hoja.
Ripoti iliyotolewa na wataalamu huru waliochunguza ajali hiyo inaeleza kuwa Hammarskjold aliuawa baada ya kunusurika kwenye ajali hiyo. Kumekuwa na taarifa kuwa ndege hiyo ilishambuliwa.
Jopo hilo linaloongozwa na Chande linatarajia  kuanza kazi mara moja na kwamba litakuwa na jukumu la kupitia nyaraka zote, ikiwamo ripoti ya kurasa 99 iliyoandaliwa na wataalamu wa awali waliochunguza mazingira ya ajali hiyo.

Related Posts:

  • WANACHAMA 100 WA BOKO HARAM WAUAWA   jeshi la Nigeria Jeshi la Nigeria linasema kuwa limewaua zaidi ya wanamgambo 100 wa kundi la Boko Haram kufuatia shambulizi la wapiganaji hao siku ya ijumaa kazkazini mashariki mwa jimbo la Borno. Vikosi vya ser… Read More
  • Alichokiandika Steve Nyerere kuhusu kujiuzulu uongozi Bongo Movie.   Kupitia mtandao wa picha yaani Instagram aliyekuwa Rais wa Bongo Movie Unity,Steve Nyerere  leo ametangaza kujiuzulu nafasi hiyo kwenye klabu hiyo ya Bongo Movie huku akishindwa kuweka sababu iliyomfanya kujiu… Read More
  • WAATHIRIWA WA MABOMU MBAGALA WALALAMIKA Nyumba iliyoharibiwa na bomu kama inavyoonekana. Mkutano kati ya waandishi habari na Waathirika wa Mabomu Mbagala, ambao umefanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mbagala Kuu ,jijini Dar-Es-Salaam mapema leo . Waathi… Read More
  • Shearer asema Welbeck atang'ara Arsenal  Mshambuliaji wa Arsenal Danny Wellbeck kushoto  Mshambuliaji mpya wa kilabu ya Arsenal Danny Welbeck anaweza kufunga mabao 25 kwa msimu mmoja ,hayo ni matamshi ya aliyekuwa … Read More
  • MFUNGWA AKUTWA NA SIMU MWILINI  Tatizo la kuingiza bidhaa kimagendo ndani ya magereza ya Kenya imekuwa kero kubwa kwa maafisa wa magereza. Kwa baadhi ya watu simu ya mkononi ni kifaa tu cha mawasIliano ilihali kwa wengine ni kifa ambacho kinaweza … Read More

0 comments:

Chapisha Maoni