JUMLA ya Watanzania 578 wamekamatwa na kufungwa katika magereza ya nchi 
mbalimbali kwa makosa ya kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.
Akiahirisha mkutano wa sita wa Bunge la 11 mjini Dodoma juzi, Waziri 
Mkuu Kassim Majaliwa, alitaja nchi ambazo Watanzania hao wamefungwa kuwa
 ni pamoja na China (200), Brazil (12), Iran (63), Ethiopia (7) na 
Afrika ya Kusini (296).
Majaliwa pia alisema vita inayoendelea nchini dhidi ya dawa za kulevya inapaswa kuungwa mkono.
Alisema madawa ya kulevya huingia zaidi kutumia kwa njia za bandari bubu
 kupitia Bahari ya Hindi na mipakani kwa njia ya magari binafsi na 
mabasi yatokayo Kenya, Uganda na Zambia.
“Lengo la serikali ni kuwasaidia walioathirika na dawa za kulevya na 
kuwachukulia hatua kali wale waliowaathiri - wauzaji na wasambazaji," 
alisema Majaliwa.






 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Chapisha Maoni