Watu waliokuwa na silaha wameushambulia msafara uliokuwa umewabeba wafungwa kaskazini mwa mji mkuu wa Iraq, Baghdad, na kusababisha makabiliano makali na majeshi. Wafungwa zaidi ya 50 na wanajeshi kumi wameuawa katika shambulizi hilo lililodhihirisha hali ya kutokuwa na amani nchini Iraq. Hii ni hata baada ya wabunge kumchagua leo mwanasiasa kigogo wa Kikurdi Fouad Massoum kuwa rais mpya. Massoum mwenye umri wa miaka 76, alipata kura 211 kati ya 228 na sasa anachukua nafasi ya Jalal Talaban ambaye mihula yake miwili ya uongozi wa miaka kumi imekamilika. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon aliwasili nchini humo mapema leo akiwaomba wabunge "kutafuta msimamo wa pamoja" ili waweze kuutatua uasi unaofanywa na kundi la itikadi kali za kiislamu linalojiita Dola la Kiislamu, pamoja na wanamgambo wa Kisunni ambao wameiteka miji kadhaa ya kaskazini na magharibi mwa Iraq. Akizungumza pamoja na Waziri Mkuu wa Iraq Nuri al-Maliki, Ban amesema Iraq inakabiliwa na "kitisho kikubwa, lakini kinachoweza kutatuliwa kama itaunda serikali inayowahusisha viongozi wa matabaka mengi.
Alhamisi, 24 Julai 2014
Home »
» Ban Ki Moon asema Iraq inapaswa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa
Ban Ki Moon asema Iraq inapaswa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa
Watu waliokuwa na silaha wameushambulia msafara uliokuwa umewabeba wafungwa kaskazini mwa mji mkuu wa Iraq, Baghdad, na kusababisha makabiliano makali na majeshi. Wafungwa zaidi ya 50 na wanajeshi kumi wameuawa katika shambulizi hilo lililodhihirisha hali ya kutokuwa na amani nchini Iraq. Hii ni hata baada ya wabunge kumchagua leo mwanasiasa kigogo wa Kikurdi Fouad Massoum kuwa rais mpya. Massoum mwenye umri wa miaka 76, alipata kura 211 kati ya 228 na sasa anachukua nafasi ya Jalal Talaban ambaye mihula yake miwili ya uongozi wa miaka kumi imekamilika. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon aliwasili nchini humo mapema leo akiwaomba wabunge "kutafuta msimamo wa pamoja" ili waweze kuutatua uasi unaofanywa na kundi la itikadi kali za kiislamu linalojiita Dola la Kiislamu, pamoja na wanamgambo wa Kisunni ambao wameiteka miji kadhaa ya kaskazini na magharibi mwa Iraq. Akizungumza pamoja na Waziri Mkuu wa Iraq Nuri al-Maliki, Ban amesema Iraq inakabiliwa na "kitisho kikubwa, lakini kinachoweza kutatuliwa kama itaunda serikali inayowahusisha viongozi wa matabaka mengi.
Related Posts:
Paul Makonda Afunguka Kuitwa na Bunge Kwa Ajili ya Kuhojiwa Home Siasa Paul Makonda Afunguka Kuitwa na Bunge Kwa Ajili ya Kuhojiwa Paul Makonda Afunguka Kuitwa na Bunge Kwa Ajili ya Kuhojiwa Siasa … Read More
Tundu Lissu Abaini Mbinu Chafu kwa Chama Fulani Kuweka Mgombea Urais TLS..!!! Mwanasheria Mkuu wa Chadema na mbunge wa Singida Mashariki kupitia chama hicho, Tundu Lissu amezungumzia hatua yake ya kujitosa kuwania urais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS). Mosi, Lissu amesema amep… Read More
Majaliwa Afunguka Issue ya Madawa ya Kulevya Inayoratibiwa na Makonda.. JUMLA ya Watanzania 578 wamekamatwa na kufungwa katika magereza ya nchi mbalimbali kwa makosa ya kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya. Akiahirisha mkutano wa sita wa Bunge la 11 mjini Dodoma juzi, Wazir… Read More
Baada ya Kutoka Selo Kwa Dhamana Hii Ndio Post ya Kwanza Aliyoandika Wema Sepetu Instagram Inawezekana kama wewe ni shabiki wa Wema Sepetu ulikua na hamu sana ya kujua post yake ya kwanza kwenye mitandao ya kijamii itahusu nini baada ya kuachiwa kwa dhamana na Mahakama kufuatia sakata la dawa za kulevya… Read More
40 ya Nillan: Wolper Achafua Hali ya Hewa, Atoa Povu Hadharani Mbele ya Wageni WAKATI sherehe ya kutimiza 40 kwa mtoto wa Diamond na Zari, Nillan ikiendelea, staa wa Bongo Movies, Jackline Wolper Massawe amekerwa na wanaomsema vibaya Zari na kuamhua kuwafungukia hadharani akitoa povu lake mbele ya… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni