Watu waliokuwa na silaha wameushambulia msafara uliokuwa umewabeba wafungwa kaskazini mwa mji mkuu wa Iraq, Baghdad, na kusababisha makabiliano makali na majeshi. Wafungwa zaidi ya 50 na wanajeshi kumi wameuawa katika shambulizi hilo lililodhihirisha hali ya kutokuwa na amani nchini Iraq. Hii ni hata baada ya wabunge kumchagua leo mwanasiasa kigogo wa Kikurdi Fouad Massoum kuwa rais mpya. Massoum mwenye umri wa miaka 76, alipata kura 211 kati ya 228 na sasa anachukua nafasi ya Jalal Talaban ambaye mihula yake miwili ya uongozi wa miaka kumi imekamilika. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon aliwasili nchini humo mapema leo akiwaomba wabunge "kutafuta msimamo wa pamoja" ili waweze kuutatua uasi unaofanywa na kundi la itikadi kali za kiislamu linalojiita Dola la Kiislamu, pamoja na wanamgambo wa Kisunni ambao wameiteka miji kadhaa ya kaskazini na magharibi mwa Iraq. Akizungumza pamoja na Waziri Mkuu wa Iraq Nuri al-Maliki, Ban amesema Iraq inakabiliwa na "kitisho kikubwa, lakini kinachoweza kutatuliwa kama itaunda serikali inayowahusisha viongozi wa matabaka mengi.
Alhamisi, 24 Julai 2014
Home »
» Ban Ki Moon asema Iraq inapaswa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa
Ban Ki Moon asema Iraq inapaswa kuunda serikali ya umoja wa kitaifa
Watu waliokuwa na silaha wameushambulia msafara uliokuwa umewabeba wafungwa kaskazini mwa mji mkuu wa Iraq, Baghdad, na kusababisha makabiliano makali na majeshi. Wafungwa zaidi ya 50 na wanajeshi kumi wameuawa katika shambulizi hilo lililodhihirisha hali ya kutokuwa na amani nchini Iraq. Hii ni hata baada ya wabunge kumchagua leo mwanasiasa kigogo wa Kikurdi Fouad Massoum kuwa rais mpya. Massoum mwenye umri wa miaka 76, alipata kura 211 kati ya 228 na sasa anachukua nafasi ya Jalal Talaban ambaye mihula yake miwili ya uongozi wa miaka kumi imekamilika. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon aliwasili nchini humo mapema leo akiwaomba wabunge "kutafuta msimamo wa pamoja" ili waweze kuutatua uasi unaofanywa na kundi la itikadi kali za kiislamu linalojiita Dola la Kiislamu, pamoja na wanamgambo wa Kisunni ambao wameiteka miji kadhaa ya kaskazini na magharibi mwa Iraq. Akizungumza pamoja na Waziri Mkuu wa Iraq Nuri al-Maliki, Ban amesema Iraq inakabiliwa na "kitisho kikubwa, lakini kinachoweza kutatuliwa kama itaunda serikali inayowahusisha viongozi wa matabaka mengi.
Related Posts:
VIONGOZI WATUMIA MADARAKA YAO KUJINUFAISHA Mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi (katikati) akifungua semina ya majadiliano kati ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma na wanahabari waliojadili rasimu ya Sheria Mpya ya Kudhibiti Mgongano wa … Read More
RATIBA LIGI KUU BARA 2014/2015 HII HAPA Kocha … Read More
Israel na Hamas waendelea na mapigano Mgogoro kati ya Israel na Palestina unaendelea. Pande zote mbili zimekuwa zikishambuliana kwa maroketi. Wakati huo huo, Misri inataka mazungumzo ya kuleta amani yaanze tena. Hali ya wasiwasi imerejea t… Read More
HATIMA YA TORRES CHELSEA;HIKI NDICHO ALICHOKISEMA Fernando Torres amemaliza kipindi kigumu kabisa cha miaka mitatu na nusu kwenye maisha yake ndani ya klabu ya Chelsea baada ya kukubali kuondoka katika timu hiyo. Fernando alijiunga na Chelsea mnamo mwaka 2011 January kw… Read More
Na hii ni nyingine tena! Wasanii walioandamana nusu uchi Nairobi Kenya. Siku hizi ishu ya kuvua nguo kuonyesha msisitizo au kulipigia kelele jambo flani imekua kawaida, yani wengi wameitumia hii njia kufikisha malalamiko yao na mfano mzuri ni hivi karibuni kwa Wanafunzi wa kike kwenye … Read More
0 comments:
Chapisha Maoni