Ijumaa, 16 Oktoba 2015

BAADA YA KUJITOA CCM BAKOZI JUMA MWAPACHU ATOA MPYA..ADAI HATA NYERERE ANGEKUWEPO ANGEJITOA CCM

Siku moja baada ya kutangaza kujitoa CCM, kada mkongwe wa chama hicho, Balozi Juma Mwapachu amesema uamuzi alioufanya ni sahihi ambao hata Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere angekuwa hai angeufanya kwa sasa.

Balozi Mwapachu alieleza hayo jana katika mahojiano maalumu na kuongeza kuwa chama chake cha zamani kimepoteza mwelekeo kwa kuwa kinara wa kuvunja katiba na taratibu kitendo ambacho Nyerere alikichukia katika maisha yake.

Alisema anafahamu fika kuna watu watakosoa uamuzi wake huo lakini hatababaishwa na maneno yao na atasimamia msimamo wake huo huku akieleza kuwa anajisikia amani kujitoa katika siku ya kumbukumbu ya miaka 16 ya kifo cha Nyerere.

Mwapachu alitangaza kujitoa CCM juzi akisema kilivunja taratibu wakati wa mchakato wa uteuzi wa mgombea wa urais uliofanyika Julai ambao Dk John Magufuli alichaguliwa.

“Nimefanya makusudi kujitoa wakati huu kwa sababu hata Nyerere mwenye angekuwapo hai leo hii angefanya uamuzi kama niliofanya. Hata yeye alikuwa ameshachoshwa na chama chake kwa uvunjaji wa kanuni, taratibu na katiba na alikwishaona kuwa kinaanza kupitwa na wakati.”

Alisema mengine yanayojitokeza kwa sasa ndani ya CCM yanaonyesha bayana kuwa chama hicho hakiendi na wakati na kilijisahau na kuendesha mambo kama kipo kwenye mfumo wa chama kimoja wakati ni wa vyama vingi.

Alisema CCM ya sasa siyo ile aliyojiunga nayo akiwa chuo kikuu, ndiyo maana amejitoa kutokana na kutekwa na watu wachache ambao humpiga vita mtu ambaye si mwenzao.

LULU, WEMA WAFIKA PABAYA..KISA UHUSIANO NA DAIMOND ..

Pamoja na wenyewe kudai hawajui kilichotokea, mastaa wawili wenye sura za mauzo kunako sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Wema Isaac Sepetu, kwa sasa wanadaiwa kufikia pabaya kufuatia bifu zito linalofukuta kati yao.

Habari za mjini zinadai kwamba, Wema amekuwa akishtushwa na kuchukizwa na kitendo cha Lulu kuwa upande wa aliyewahi kuwa mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kiasi cha kwenda nyumbani kwake, Madale-Tegeta jijini Dar, usiku wa manane na kujiachia na jamaa huyo anavyotaka.

“Kama mtakumbuka, kabla ya kifo cha Kanumba (Steven), Wema na Lulu walikuwa ni mashosti kama ilivyokuwa kwa Wema na Snura (Mushi) au Wema na Kajala (Masanja) au Wema na Aunt (Ezekiel).

“Lakini baada ya jamaa (Kanumba) kuondoka na kisa kizima cha Lulu ndipo Wema akavunja urafiki na Lulu kwa sababu Kanumba aliwahi kuwa ‘mtu’ wa Wema kama ilivyo kwa Diamond.

“Ulipita ukimya wa muda mrefu bila Wema na Lulu kuwa mashosti zaidi ya salamu.

“Lakini mambo yalianza tena kuwa mabaya baada ya Lulu kumponda Wema alipokuwa akigombea Ubunge wa Viti Maalum kupitia CCM (Chama Cha Mapinduzi).

“Sasa hivi ishu ni kitendo cha Lulu kujiachia na Diamond kwenye birthday ya Rome Jones (binamu na DJ wa Diamond) kisha ile pati ya birthday Diamond kuifanyia nyumbani kwake huku (Lulu) akitupia picha za mafumbo yaliyoelekezwa kwa Wema.

“Hicho ndicho kinachoendelea na unaambiwa hali ni tete mno,” kilisema chanzo hicho ambacho ni mtu wa karibu wa mastaa hao.

Baada ya kupata ‘ubuyu’ kamili, Amani lilimtafuta Wema na kummwagia data ambapo alionesha kushtushwa na kudai kwamba hata yeye anashangaa ni nini kimetokea.

Kwa upande wake Lulu hakupatikana hewani lakini kwa mujibu wa mahojiano aliyofanya hivi karibuni juu ya uhusiano wake na Wema, mwanadada huyo alikiri kuwa rafiki wa Wema kitambo hicho lakini akasema hajui ni nini kilichotokea zaidi ya kwamba huwa wanasalimiana tu wanapokutana.

Kabla ya mambo kwenda mrama, Lulu na Wema walikuwa mashosti wakubwa ambapo gazeti hili liliwahi kuwashuhudia wakiwa lokeshi na kulala pamoja chumba kimoja kama mtu na dada au mtu na mdogo wake.

Chanzo: GPL

HABARI KUHUSU HELIKOPTA YA CCM ILIYOANGUKA MBUGANI IKIWA NA MBUNGE DEO FILIKUNJOMBE

Usiku wa kuamkia leo October 16 2015 majukwaa  ya siasa Tanzania yametawaliwa na ajali ya Helikopta ambayo imeanguka na kulipuka kwenye mbuga ya Wanyama ya Selous ambapo Waziri wa maliasili na utalii Lazaro Nyalandu alithibitisha kwamba mmoja wa waliokuwemo ndani ni Mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe (CCM).

Kupitia  ukurasa  wake  wa  Twitter,Nyalandu  aliandika;
"Tumetuma vikosi vya maafisa na maaskari katika eneo la Selous kulikotokea ajali ya helikopta katika harakati za uokozi, ajali ya helikopta imetokea katika kitalu R3 ndani ya mbuga ya Selous na mashuhuda wanasema ilianguka na kulipuka ng’ambo ya mto Ruaha

"Mashuhuda wa ajali ya helikopta iliyotokea Selous walikuwa kitalu R2 na walishuhudia ikianguka na kulipuka ng’ambo ya mto Ruaha Kitalu R3, Maafisa na Maaskari wanaelekea eneo la tukio kutokea Msolwa na Matambwe na tumeagiza vikosi vilivyo kwenye doria Selous kushiriki uokoaji

"Mashuhuda wa ajali ya helikopta Selous walikuwa Kitalu R2 wanasema ilianguka baada ya majira ya saa 12 jioni na kulipuka, serikali kupitia wizara ya maliasili na utalii inachukua hatua zote kuwafikia wahanga na majeruhi wa ajali ya helikopta Selous usiku huu

"Nimeagiza section 2 zenye askari 16 kutoka Matambwe na Msolwa (Selous) kwenda eneo la tukio, RPC Morogoro na mkuu kanda ya Msolwa (Selous) wanashirikiana, hatujui kitakachokuwa kimewapata wasafiri ndani ya helikopta iliyoanguka akiwepo Mh, Filikunjombe, tuungane kuwaombea kwa Mungu"

Katika taarifa nyingine kutoka upande wa CCM iliyotolewa na naibu waziri wa mawasiliano sayansi na teknolojia January Makamba mida ya saa sita usiku ilisema:  "Tumesikia habari za chopa kuanguka huko Selous. Mungu aepushe kusiwe na majeruhi. Chopa zote zinazotumiwa na CCM kwenye kampeni ziko salama"

Baadae aliandika :"Kwakuwa ilisemekana kuwa chopa ya kampeni ya CCM imeanguka, tulifuatilia/kubaini/kuripoti kuwa tulizokodi kama Chama hakuna iliyoanguka". Hiyo ndio ilikua tweet ya mwisho kuandikwa na January Makamba usiku lakini badae aliretweet kilichoandikwa na Waziri Nyalandu na Zitto Kabwe.

Zitto aliandika: "Naomba utulivu.(1) ajali ya helkopta imethibitishwa (2) kuwaka hakujathibitishwa (3) ndugu yangu Deo alikuwamo (4) hakuna uthibitisho wa madhara, naomba utulivu mpaka tupate taarifa rasmi zilizothibitishwa na mamlaka husika, naomba sana hilo ili kuepuka sintofahamu"

BAADHI YA VITUKO VILIVYOPO NDANI YA DAFTARI LA WAPIGA KURA..PICHA ZIMEPIGWA JANA WAKATI UKAWA WAKIONGEA NA WAANDISHI WA HABARI

Huyu  Kaandikishwa  kwa  jina  la  GGGHUH  GGJGJHGHG GGHGGGHG

Mwangalie  vizuri  mzungu    na  majina  yake. Picha  ya  pembeni  kulia  ni  kitu  cheusi  na  siyo  sura  ya  mtu
Angalia  Jina  na  hiyo  picha. Kwa  kuiangalia  sidhani  kama  ni  picha  ya  binadamu
Tazama  majina  na  picha
Hizi  picha  mbili  za  kulia  sio  za  binadamu. Moja  ni  kama  ya  mlango, nyingine  ni  weusi tu  unaonekana

JERRY SLAA AANDIKA HAYA KUHUSU AJALI YA HELIKOPTA YA CCM..KUMBE BABA YAKE NAYE YUMO KATIKA AJALI HIYO


Jerry Silaaa Ameandika Haya Katika Ukurasa Wake wa Instagram

@jerrysilaa - Baba yangu Capt.William Silaa akiwa na Mhe.Deo Filikunjombe na abiria wengine walipata matatizo ya engine ya helicopter 5Y-DKK jana jioni wakitokea Dar kuelekea Ludewa. Taarifa za mwisho ilionekana imeanguka kwenye msitu wa Selous. Hakuna mawasiliano ya simu. Usiku kucha vyombo vyote vya serikali vimeendelea na jitihada za kufika eneo la tukio na jitihada kubwa zaidi zinaendelea asubuhi hii.
Nawaomba wote kuwa watulivu kwani jambo hili linahitaji umakini wa hali ya juu na ushirikiano wa taasisi nyingi za wizara tofauti.
Tuwaombee wote Mungu awanusuru.

LOWASA AIONYA TUME YA UCHAGUZI KWA KINACHOENDELEA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU OCT 25

Mgombea urais anaesubiri kuapishwa Edward Lowassa akiwa katika jimbo la Magu ameitaka tume ya uchaguzi kuwa makini kama kweli tume hiyo iko huru la sivyo wataiingiza nchi katika matatizo makubwa ambayo hayajawahi kutokea nchini.

Lowassa amewataka tume kuwa makini pasipo kuyumbishwa kwa kuwa amani ya nchi hii iko mikononi mwao.Alisema anasikitishwa sana na maelezo yanayotolewa na tume hiyo huku akihoji wapi uhuru wa tume hiyo kama walivyodai mwanzo kuwa wako huru.

Lowassa pia ameitaka serikali ya CCM kutocheza na amani ya nchi hii.

Alhamisi, 15 Oktoba 2015

ZARI NA DAIMOND ETI BASI TENA..BIASHARA KWISHNEY

BIASHARA imekwisha! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia ‘kapo’ ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kudaiwa kuwa waliweka misingi ya penzi zito ili Diamond apate mtoto hivyo baada ya mrembo huyo kujifungua Latifah ‘Tiffah’ miezi miwili iliyopita, penzi halitakuwa motomoto kama zamani, Risasi Jumamosi lina ‘full’ stori.

Chanzo cha uhakika kilicho karibu na wawili hao, kimesema makubaliano ya awali baina ya wazazi hao, yalikuwa ni kwa mwanamke huyo raia wa Uganda, kumzalia mtoto Diamond ambaye alikuwa akisaka ubaba kwa udi na uvumba.

TUJIUNGE NA CHANZO
“Wote mnajua jinsi Diamond alivyokuwa akihangaika kupata mtoto, maana wapenzi wake wote wa awali hawakuweza kumzalia. Sasa alipokutana na Zari ambaye tayari alikuwa na watoto, wakakubaliana kwa masharti kuwa ndani ya muda f’lani, amzalie.

“Sasa ndiyo ikawa hivyo, baada ya Tiffah kuzaliwa, kila mtu sasa yupo huru kufanya yake, ndiyo maana Zari amerudi kwake Afrika Kusini ‘Sauz’ na hawezi kuja kuendelea kuishi na Diamond kama wakati ule wa ujauzito.
“Kule Sauz, Zari anaendelea na biashara zake na nimesikia kwa sasa anaandaa Zari All White Party kama ile aliyoifanya Mlimani City hapa Bongo,” kilisema chanzo chetu.

Msanii chipukizi wa lebo ya Wasafi Classic Baby ‘WBC’ aitwaye Harmonizer akilishwa keki na Rose.

KWA NINI HAWEZI KURUDI?
Chanzo hicho kiliendelea kutoboa siri kwamba, pamoja na makubaliano ya kuzaa, lakini pia mazingira ya sasa ya makazi ya Diamond hayatoi nafasi kwa mwanamke huyo mwenye fedha ambaye pia ni msanii, kuweza kuishi.
“Sasa hivi pale nyumbani kwa Diamond kumejaa, imekuwa familia kubwa. Maana kuna mjomba wake Diamond anaishi pale, dada zake wawili, Esma na Queen Darleen wanaishi pale. Mama yake Diamond (Sanura Kasim) yupo pale.
“Haya, achana na ndugu wengine. Lakini pia kuna wasichana wa kazi wawili na mlinzi mmoja. Sasa kwa mtu kama Zari ambaye maisha yake ni ya kisupastaa hawezi kuishi kwenye nyumba yenye watu wengi hivyo.”

ZARI ANAOGOPA UMBEYA
“Pia inasemekana Zari hataki kuishi na wifi zake kwa sababu anaogopa umbeya. Hata wakati ule alipokuwa mjamzito mpaka kujifungua, hakuwa mtu wa kujichanganya nao sana. Alikuwa mtu wa peke yake peke yake tu.”

HAKUNA TENA MAPENZI?
“Taarifa nilizonazo ni kuwa, Diamond na Zari watakuwa wanaendelea na uhusiano wao wa kimapenzi lakini si ule wa kama awali. Ila wataendelea kuwa watu waliozaa mtoto na maisha ya Tiffah yataendelea kuwa kwa mama yake hadi hapo watakapoamua vinginevyo. Zari anaweza kuja Bongo na Diamond anaweza kwenda Sauz kwa Zari.”
“Zari hataki kuishi Tanzania, anataka Tiffah aishi na ndugu zake kule Sauz hadi akue na kuanza masomo. Kwa hiyo usitegemee ule ukaribu kama wa mwanzo.”

KUHUSU DIAMOND!
Jitihada za kumpata Diamond ili aweze kuzungumzia suala hilo ziligonga mwamba ikielezwa kuwa yupo nchini Marekani katika shughuli za kimuziki. Hata alipotumiwa meseji kwa njia ya Mtandao wa WhatsApp hakujibu.
Hata hivyo, mtu wake wa karibu ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazetini, alitatizwa na suala hili akisema:

“Dah! Wabongo bwana! Ninachojua mimi ni kuwa, bado watakuwa wapenzi japokuwa siwasemei maana Diamond naye haaminiki sana. Si unajua ameshapata mtoto, lolote linaweza kutokea.
“Ila Diamond akimhitaji Zari aje Tanzania anaweza kuja, akitaka aende Sauz atakwenda kwa sababu Tiffah lazima alelewe na wazazi wote.
“Halafu lazima ujue kwamba, Zari ni mfanyabiashara, ana biashara zake Afrika Kusini na Uganda. Kwa hiyo siyo mtu ambaye unaweza kumtegemea akae sehemu moja tu.”