WATAHINIWA 74,920 leo wanaanza kufanya mtihani wa kuhitimu Kidato cha Sita katika shule mbalimbali nchini huku watahiniwa 11,597 wakifanya mtihani wa Ualimu.
Ofisa Habari wa Baraza la Mitihani (NECTA), John Nchimbi amesema kuwa mtihani wa kidato cha sita unaanza leo hadi Mei 19, mwaka huu. Nchimbi alisema kati ya watahiniwa hao waliosajiliwa, watahiniwa 65,610 ni watahiniwa wa Shule huku watahiniwa wa Kujitegemea wakiwa 9,310.
“Kati ya watahiniwa wa shule 65, 610, watahiniwa wasichana ni 24,549 na wavulana ni 41,061 huku watahiniwa wa kujitegemea wasichana wakiwa ni 3,176 na wavulana ni 6,134,” alisema Nchimbi.
Kwa upande wa mtihani wa ualimu, Nchimbi alisema kati ya watahiniwa 11,597 watakaofanya, watahiniwa 10,942 wanafanya Ualimu Daraja A na watahiniwa 654 wanafanya mtihani wa Stashahada ya Sekondari na mmoja anafanya Stashahada ya Ufundi.
Jumapili, 1 Mei 2016
Home »
» 75000 WAFANYA MTIHANI KIDATO CHA 6 LEO
75000 WAFANYA MTIHANI KIDATO CHA 6 LEO
Related Posts:
AJARI YA GARI WALIYOPATA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJIRI AKIWEMO BAHATI BUKUKU. Gari lenye namba IT 7945 Toyota Nadia likiendeshwa na EDSON MWAKABUNGU (31) mkazi wa Tabata Dar es Salaam liliacha njia na kugonga gema na kusababisha majeraha kwa watu watatu baada ya kugongwa na gari jingine … Read More
Taarifa rasmi kutoka club ya Chelsea kuhusu Didier Drogba. Utakua uliziona tu zile headlines za mitandao na magazeti mbalimbali duniani kuhusu uwezekano wa staa huyu wa soka Didier Drogba kurejea kuichezea Chelsea baada ya Jose Mourinho kuonyesha nia ya kumrudisha. Sasa … Read More
Matokeo ya tuzo za AFRIMMA 2014 alizokua anawania Diamond Marekani. Zinaitwa African Muzik Magazine Awards ambapo za mwaka huu 2014 zimetolewa huko Eisemann center Texas Marekani na kuhudhuriwa na mastaa mbalimbali akiwemo Diamond wa Tanzania ambae pia alikua mmoja wa wanaowania t… Read More
Video mpya ya Barnaba aliyoonekana na mke wake ndio hii. Hii single inaitwa ‘Wahaladee’ ambayo ni miezi kadhaa imepita tangu utoke rasmi kwenye Radio lakini July 25 2014 Watanzania wameletewa video yake ambayo imeongozwa na Nick Dizzle ambapo kingine kikubwa kwenye hii video n… Read More
Dully Sykes anakualika kusikiliza single yake mpya hapa inaitwa ‘Togola’ Mara yake ya mwisho kusikika na single mpya kwenye Radio ilikua June 2013 na ilikua ni ‘Kabinti special’ ambayo video yake ilionekana ndani ya muda mfupi sana toka iachiwe na hiyo ni kutokana na video hiyo kutajwa kwamba … Read More
0 comments:
Chapisha Maoni