Januari 29, 2009 Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda alimwaga machozi Bungeni na kufikia hatua ya kutoa kauli kali juu ya wanaofanya vitendo vya kikatili vya mauaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi kwamba “wanaoua albino nao wauawe”
Hadi sasa idadi ya Watanzania wanaosubiri kunyongwa imekuwa ikiongezeka siku hadi siku na kufikia 465 kutokana na hukumu ya kifo kutotekelezwa nchini tangu mwaka 1994.
Ripoti ya Mpango wa Kujitathmini Kuhusu Hali ya Utekelezaji wa Haki za Binadamu (UPR), unaotekelezwa kwa mara ya pili nchini Tanzania, umeonesha ongezeko la mahabusu 465 wanaosubiri adhabu ya kifo, kati yao wanaume ni 445 huku wanawake wakiwa 20 baada ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, kubainisha hakuna hukumu yoyote ya kifo iliyosainiwa na Rais Dk. Magufuli ili kutekelezwa tangu Oktoba mwaka jana alipoingia madarakani.
Hata hivyo Ofisa Uchunguzi Mkuu wa Tume hiyo Philemon Mponezya, amesema Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, inaitaka Serikali kufuta adhabu ya kifo kwa kuwa haitekelezeki ingawa kumekuwa na mvutano mkali kati yao na baadhi ya asasi hasa zinazohusika na haki za walemavu wa ngozi zikipinga vikali kufutwa kwa adhabu hiyo.
“Watetezi wengi wa haki za binadamu nchini Tanzania wanataka adhabu hiyo ifutwe kwa kuwa ni kinyume cha haki za binadamu na kwa Tanzania, imekuwa mbaya zaidi kwa baadhi ya wahukumiwa waliosubiri zaidi miaka 20 bila hukumu dhidi yao kutekelezwa, jambo hili linawaathiri kisaikolojia”. Amesema Mponezya.
Jiunge nasi
Insta@ubuyuhotz , fb@ubuyuhotz .
Jumapili, 1 Mei 2016
Home »
» IDADI YA WANAOSUBIRI KUNYONGWA TANZANIA YAONGEZEKA
IDADI YA WANAOSUBIRI KUNYONGWA TANZANIA YAONGEZEKA
Related Posts:
MKE WA KIONGOZI IS AKAMATWA Kiongozi wa IS Abu Bakr al-Baghdadi Vikosi vya usalama nchini Lebanon vimemkamata mkewe kiongo… Read More
Al Shabaab waua 36 Mandera,Kenya Wapiganaji wa Al Shabab&n… Read More
Man city wazidi kupanda Wachezaji wa Klabu ya Man city Kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini amesema ushindi wa timu yake dhidi ya Southampton unadhi… Read More
Aliyewakosoa Sasha na Malia ajiuzuluSasha na Malia walikosolewa kwa kuvalia sketi fupi mbele ya umati katika White House Mfanyakazi katika chama cha Republican nchini Marekani amejiuzulu baada ya kukosolewa kwa kuwatuhumu wanawe Rais wa Marekani Barack Obam… Read More
Obama na vurugu za Marekani &nb… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni