Januari 29, 2009 Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda alimwaga machozi Bungeni na kufikia hatua ya kutoa kauli kali juu ya wanaofanya vitendo vya kikatili vya mauaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi kwamba “wanaoua albino nao wauawe”
Hadi sasa idadi ya Watanzania wanaosubiri kunyongwa imekuwa ikiongezeka siku hadi siku na kufikia 465 kutokana na hukumu ya kifo kutotekelezwa nchini tangu mwaka 1994.
Ripoti ya Mpango wa Kujitathmini Kuhusu Hali ya Utekelezaji wa Haki za Binadamu (UPR), unaotekelezwa kwa mara ya pili nchini Tanzania, umeonesha ongezeko la mahabusu 465 wanaosubiri adhabu ya kifo, kati yao wanaume ni 445 huku wanawake wakiwa 20 baada ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, kubainisha hakuna hukumu yoyote ya kifo iliyosainiwa na Rais Dk. Magufuli ili kutekelezwa tangu Oktoba mwaka jana alipoingia madarakani.
Hata hivyo Ofisa Uchunguzi Mkuu wa Tume hiyo Philemon Mponezya, amesema Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, inaitaka Serikali kufuta adhabu ya kifo kwa kuwa haitekelezeki ingawa kumekuwa na mvutano mkali kati yao na baadhi ya asasi hasa zinazohusika na haki za walemavu wa ngozi zikipinga vikali kufutwa kwa adhabu hiyo.
“Watetezi wengi wa haki za binadamu nchini Tanzania wanataka adhabu hiyo ifutwe kwa kuwa ni kinyume cha haki za binadamu na kwa Tanzania, imekuwa mbaya zaidi kwa baadhi ya wahukumiwa waliosubiri zaidi miaka 20 bila hukumu dhidi yao kutekelezwa, jambo hili linawaathiri kisaikolojia”. Amesema Mponezya.
Jiunge nasi
Insta@ubuyuhotz , fb@ubuyuhotz .
Jumapili, 1 Mei 2016
Home »
» IDADI YA WANAOSUBIRI KUNYONGWA TANZANIA YAONGEZEKA
IDADI YA WANAOSUBIRI KUNYONGWA TANZANIA YAONGEZEKA
Related Posts:
WCB Wabadilike Uimbaji Nashangaa kuona wasanii wote wanaimba key moja mwisho wa siku haitambuliki huyu ni nani sababu wanaigana kama wataendelea hivi watachokwa hakuna anayetaka kubadika. Baada yakuja huyo Lava Lava nikazani anakuja na key tof… Read More
Kajala Aibuka na Haya Kuhusu Wema Sepetu..Adai Hata Mwanae ni Shahidi..!!! TASNIA ya filamu nchini imepambwa na wasanii wa kike wenye urembo unaovutia macho na hakika kwenye orodha ya waingizaji wenye kipaji, uwezo na mvuto huwezi kumuacha, Kajala Masanja. Huyu ndiyo bosi wa kampuni ya Kaja… Read More
Vita Ya Malipo Kiduchu Haijawahi Kumuacha Modo Salama! AMANDA Swartbooi moja kati ya wauza nyago katika video Afrika akitokea Afrika Kusini. Amanda ametokea kujizolea umaarufu kwa kipindi kifupi cha mwaka jana ambapo ametokea katika video kadhaa Afrika ikiwemo Coolest Kid ya D… Read More
Friji Lateketeza Jengo la Ghorofa 27 kwa Muda wa Dakika 15..!!! MOTO uliozuka kwenye jengo la ghorofa 27 lililoko London Magharibi kwa dakika 15 baada ya friji kulipuka, itakuwa ni moja ya ajali mbaya kupata kutokea katika historia ya nchi hii huku kukiwa na hofu ya kutokuw… Read More
Wema Sepetu Amzimikia Rayvanny Amtabiria Makubwa Tuzo za BET RayVanny ni msanii pekee kutoka Tanzania na Afrika Mashariki ambaye anatuwakilisha kwenye tuzo za BET zitakazofanyika Marekani baadaye mwezi huu akiwania Viewers Choice Awards ama (Pendekezo la Mashabiki ama watazamaji) hu… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni