SERIKALI ya Awamu ya Tano imeanza kutekeleza kwa vitendo azma yake ya kujenga uchumi unaotegemea viwanda baada ya kuzindua ujenzi wa mradi maalumu wa uwekezaji wa viwanda mkoani Morogoro ili kukuza uchumi na kuongeza ajira nyingi kwa vijana nchini.
Utekelezaji huo ni kutokana na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage juzi kuzindua eneo maalumu la ujenzi wa miradi ya uwekezaji la Star City katika Manispaa ya Morogoro.
Eneo hilo la miradi ya uwekezaji lina ukubwa wa ekari 10,661 na lilikuwa ni shamba la mkonge Tungi Sisal Estate ambalo kwa sasa likijulikana kwa jina la Dominio Plantation Limited (DPL).
Waziri Mwijage kabla ya kuzindua eneo hilo maalumu la uwekezaji, alisema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli imeanza utekelezaji wa Tanzania kuwa nchi ya viwanda kwa kuanza na Mkoa wa Morogoro.
“Morogoro haijapendelewa isipokuwa ina historia tangu wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambapo Waziri Jamal (Amir) aliwezesha kujengwa kwa viwanda hivi hapa Morogoro,” alieleza Mwijage na kuongeza: “Morogoro ina bahati ya kuwa na sifa ya kujenga viwanda kutokana na mazingira na jiografia yake naweza kusema ina bahati ya kuzaliwa ilivyoumbwa na Mungu kuvutia uwekezaji.”
Jumapili, 1 Mei 2016
Home »
» TANZANIA YA VIWANDA KUANZIA MOROGORO
TANZANIA YA VIWANDA KUANZIA MOROGORO
Related Posts:
WASOMI WAKOSOA ASILIMIA 2% YA KODI ALIYOPUNGUZA RAIS MAGUFULI Siku moja baada ya Rais Magufuli kushusha Kodi ya Mapato ya Mshahara ( Pay as you Earn – PAYE ) kutoka asilimia 11 iliyopo sasa hadi asilimia 9. Wataalamu wa uchumi nchini wamelipokea katika mtazamo tofauti Mtaalamu wa Uchum… Read More
POLISI MATATANI KWA KUOMBA RUSHWA YA MILIONI 7 POLISI mkoani Rukwa inawashikilia askari wake wawili wa Kituo Kikuu cha Polisi wilayani Nkasi, wakituhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya zaidi ya Sh milioni 7.2 wamsaidie mtuhumiwa. Kaimu Kamanda wa Polisi wa Rukwa, Leonce … Read More
Wabunge Watwangana Ngumi Bungeni.. Wanachama wa chama tawala cha Uturuki cha AK na chama kinachoungwa mkono na Wakurdi wamepigana ngumi bunge kuhusiana na mpango kuwaondolea kinga wabunge ya kutoshitakiwa. Wabunge wakionyeshana umwamba Bungeni nchini Uturuki … Read More
PENZI la Mwanamuziki Shaa na Master Jay...Shaa Afunguka Kinachoendelea Kwa Sasa....Master J na Shaa wamekuwa kwenye uhusiano kwa miaka mingi sasa na wameendelea kuwa imara. akini pamoja na kuwa hivyo, bado uhusiano wao wa kikazi una nafasi kubwa zaidi. Hali hiyo ndiyo imemfanya Shaa kujitahidi kutofautisha … Read More
Ole Wao Wanaowapa Ujauzito Wanafunzi-Ummy Serikali imewaagiza Maafisa maendeleo ya Jamii na maafisa ustawi wa Jamii wa wilaya,kata na mikoa nchini kuwafatilia wanaume wanaowapa ujauzio wanaume wanaowapa ujauzito watoto wa shule na kuwafikisha Mahakamani. Akizungumza… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni