Daniel Anael Lema, aliyekuwa mwanafunzi wa mwaka wa nne wa shahada ya sheria katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Mt. Augustino, Tawi la Iringa (Ruaha University College - RUCO) enzi za uhai wake
Jeneza lenye mwili wa marehemu Daniel Lema kabla ya kuagwa.
Marehemu Daniel Lema akiwa hospitali baada ya kuchomwa moto na wananchi.
Ndugu wa marehemu wakiandaa jeneza kwa ajili ya mwili wa marehemu Daniel kuagwa.
Daniel Anael Lema, aliyekuwa mwanafunzi wa mwaka wa nne wa shahada ya sheria katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Mt. Augustino, Tawi la Iringa (Ruaha University College - RUCO), amefariki dunia baada ya kushambuliwa kisha kuchomwa moto na wananchi wenye hasira akidhaniwa kuwa mwizi.
Tukio hilo lilitokea Juni 24, 2014, majira ya saa 5 usiku ambapo inadaiwa kuwa Daniel alikuwa ametoka kuangalia michuano ya Kombe la Dunia, akawa anatafuta chakula cha jioni ambapo alipofika kwenye mgahawa mmoja ambao ulikuwa umefungwa, aliingia ndani ambapo binti aliyekuwa amelala ndani ya mgahawa huo, alianza kupiga kelele za mwizi zilizowakusanya wananchi wenye hasira kali.
Wananchi hao walianza kumshambulia Daniel wakiongozwa na mlinzi mmoja wa jamii ya Kimasai, baada ya kuzidiwa na kichapo wananchi hao walimmwagia mafuta ya taa na kumchoma moto kisha wote wakatoweka.
Mwanafunzi huyo aliokolewa na madereva bodaboda ambao walizima moto na kumkimbiza katika Hospitali ya Rufaa ya Iringa lakini siku kadhaa baadaye alifariki dunia.
Mwili wa marehemu umeagwa mapema leo katika hospitali hiyo tayari kwa safari ya kuelekea mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika kesho Jumatano.
Mungu na ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMINA
Jumanne, 1 Julai 2014
Home »
» JE WAJUA MWANAFUNZI CHUO KIKUU ALIYECHOMWA MOTO AFARIKI, KUZIKWA KESHO KILIMANJARO
JE WAJUA MWANAFUNZI CHUO KIKUU ALIYECHOMWA MOTO AFARIKI, KUZIKWA KESHO KILIMANJARO
Related Posts:
Mama Wema Sepetu Aonyesha Alivyoumbika Adai Mtoto wake Amechukua Kwake..Awashangaa Wanaosema Wema Ametumia Dawa Kukuza MakalioMama Wema Sepetu Ameongea na Kusema kuwa anawashangaa wale wote wanaosema mtoto wake ameongeza makalio kwa dawa wakati wanaona kabisa kuwa amerisi makalio hayo kutoka kwa mama yake...Mama huyo amekwenda mbali zaidi na kuweka … Read More
HASARA ZA KUTOFANYA MAPENZI KWA MUDA MREFUUkidumu bila tendo la ndoa muda mrefu, baadhi ya madhara madogo madogo yanaweza kujitokeza kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa kiafya karibu twende sawa katika darasa la leo Mwalimu ndio nshakuandalia vitu vitamu jisomee ili uf… Read More
Gigy Money Afunguka Kuhusu Mapicha yake ya Nusu Utupu Mtandaoni..Adai Ndio zinampatia Pesa.....Video queen aliyetokelezea kwenye video kibao za bongo Gigy Money ameamua kufunguka juu ya masinema yake. Giggy ambaye haishi vituko na kuibua mapya kila siku mitandaoni aliiambia eNewz kuwa yeye wala hajali maneno ya watu na… Read More
JPM AAGIZA ASKARI ALIYETUKANWA NA MKE WA WAZIRI APANDISHWE CHEORais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amemuagiza Kamishna wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Ernesti Mangu kumpandisha cheo mara moja askari wa Usalama Barabarani ambaye alitukanwa na Mke wa Waziri wakat… Read More
DALILI ZA MWANAMKE ANAYEKUPENDA KUTOKA MOYONIWahenga walinena kuwa “penzi ni kikohozi kulificha hauwezi” hakika wazee wetu hawakukosea Mapenzi ni hisia ambazo huwezi kuzizuia kwa namna yeyote ile kwani huanza kwa siri baina ya wawili lakini baadaye huwa sio siri tena, v… Read More
0 comments:
Chapisha Maoni